Katika majlisi ya maombolezo ya kuadhimisha shahada ya Imamu Jawad (a.s) iliyofanyika katika mji mkuu wa Senegal, Dakar, Ayatollah Reza Ramadhani — Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt (a.s) — alisisitiza: "Kufaidika na mafundisho na maneno ya Ahlul Bayt (a.s) hutusaidia katika safari ya kimatendo ya kumkaribia Mwenyezi Mungu." Amebainisha kuwa: "Maudhui yanayotolewa na Ahlul Bayt (a.s) ni ya ki-Tawhidi, yamejengwa juu ya msingi wa maumbile ya mwanadamu (fitra), na yanakubaliana kikamilifu na akili ya binadamu."