Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) -ABNA-, Hafla ya maombolezo ya Shahada ya Imamu Muhammad al-Jawad (a.s) ilifanyika kwa heshima kubwa katika Kituo cha Kiutamaduni cha Imam Ridha (a.s) kilichoko mjini Dakar, mji mkuu wa Senegal, kwa mahudhuri ya familia za Wairani wanaoishi nchini humo.
Ayatollah Reza Ramezani - Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s) - aliyepo nchini Senegal kwa mwaliko rasmi wa viongozi wa kidini wa nchi hiyo, alikuwa mzungumzaji maalumu katika hafla hiyo tukufu.
Pamoja naye, walihudhuria pia:
-
1-Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Senegal
-
2-Mshauri wa masuala ya utamaduni wa Iran
-
3-Mwakilishi wa Jāmi‘at al-Mustafā
-
4-Baadhi ya wanadiplomasia wa ubalozi wa Iran
-
5-Wawakilishi wa kiuchumi wa Iran nchini Senegal
-
6-Na baadhi ya maafisa wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt (a.s)
Mafundisho ya Ahlul Bayt (a.s) ni Njia ya Kumkaribia Mwenyezi Mungu
Katika hotuba yake, Ayatollah Ramezani alieleza kuwa:"Kununua elimu na mafundisho ya Ahlul Bayt (a.s) hutuwezesha kivitendo kumkaribia Mwenyezi Mungu. Mafundisho haya ni ya Tauhidi, yanatokana na maumbile ya mwanadamu (fitra), na yanalingana kikamilifu na akili timamu."
Sifa Tatu Muhimu za Muumini kwa Mujibu wa Imamu Jawad (a.s)
Ayatollah Ramadhani alielezea hadhira kuwa kulingana na riwaya mashuhuri kutoka kwa Imamu Jawad (a.s), muumini wa kweli anapaswa kuwa na sifa tatu:
-
Tawfiq kutoka kwa Mwenyezi Mungu – Si kila mtu mwenye muda anapata fursa ya ibada; mtu anatakiwa atafakari ni nini kinamzuia kupata tawfiq hiyo.
-
Kuwa Mnasihi wa Nafsi Yake Mwenyewe – Muislamu hapaswi kungoja nasaha kutoka kwa wengine tu, bali anapaswa kuwa na uwezo wa kujinasihi binafsi.
-
Kukubali Nasaha za Wengine – Muumini wa kweli huonesha moyo wa kupokea nasaha na maoni ya watu wengine wenye nia njema."Kuwa na sifa hizi kutatuwezesha kutoa huduma kubwa kwa dini ya Mwenyezi Mungu, lakini pia tunapaswa kuwa tayari kwa changamoto na mitihani njiani," aliongeza Ayatollah Ramezani.
Kumbukumbu ya Maombolezo
Katika sehemu ya mwisho ya hafla hiyo, bwana Ali Hashemi — mtumbuizaji wa mashairi ya maombolezo — alisoma qasida na nyimbo za huzuni kwa ajili ya kumbukumbu ya shahada ya Imamu Muhammad al-Jawad (a.s).
Your Comment