viongozi
-
Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania:
Viongozi wa Kitaifa wa JMAT-TAIFA Wajadili Ajenda za Amani na Maridhiano Jijini Arusha
Askofu Profesa Rejoice Ndalima: "Inafaa na inapendeza kwa viongozi wa kijamii na kidini kuungana ili kupunguza migawanyiko na kuondoa maneno ya chuki miongoni mwa Wananchi".
-
Jumuiya ya Al-Wefaq: Mkutano wa Waziri Mkuu wa Bahrain na Balozi wa Israeli ni “Dhalili ya Kuanguka kwa Diplomasia”
Jumuiya ya Al-Wefaq imeelezea mkutano wa Waziri Mkuu wa Bahrain na balozi wa utawala wa Kizayuni kama ishara ya kushindwa kwa diplomasia na kuendelea kwa sera ya kawaida za kawaida bila kuzingatia vipengele vya kibinadamu na kidini, na kuwatuhumu viongozi wa Bahrain kushiriki kwa kimyakimya katika “uchumi wa mauaji ya kimbari.”
-
Chanzo: Tovuti Rasmi ya Ofisi ya Ayatollah Makarim Shirazi | Je, Sheria ya Mtume (s.a.w.w) Inaruhusu Kuuawa kwa Imam Hussein (a.s)?
Kwa mujibu wa Aya ya "Tathira" (Qur’an, Ahzab: 33), Ahlul-Bayt (a.s), akiwemo Imam Hussein(as), wamesafishwa (wametakaswa) na Mwenyezi Mungu dhidi ya dhambi. Hivyo, haiwezekani Imam kuwa chanzo cha fitina au kuvunja umoja.
-
Ayatollah Ramezani Mjini Dakar: Mafundisho ya Ahlul-Bayt (a.s) ni Njia ya Kumfikia Mungu
Katika majlisi ya maombolezo ya kuadhimisha shahada ya Imamu Jawad (a.s) iliyofanyika katika mji mkuu wa Senegal, Dakar, Ayatollah Reza Ramadhani — Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt (a.s) — alisisitiza: "Kufaidika na mafundisho na maneno ya Ahlul Bayt (a.s) hutusaidia katika safari ya kimatendo ya kumkaribia Mwenyezi Mungu." Amebainisha kuwa: "Maudhui yanayotolewa na Ahlul Bayt (a.s) ni ya ki-Tawhidi, yamejengwa juu ya msingi wa maumbile ya mwanadamu (fitra), na yanakubaliana kikamilifu na akili ya binadamu."
-
JMAT Yatoa Wito kwa Viongozi wa Dini Nchini Kenya wa Kushirikiana Katika Kuwaongoza Wananchi wao ili Kuheshimiana na Kutunza Mahusiano ya Amani
Sheikh Dkt. Alhad Mussa Salum: "Wakenya ni ndugu wa Watanzania, na mbali na uhusiano wa kijamii, ni ndugu wa damu. Tunatambua kuwa mizozo hii inahusu zaidi vijana wa Kenya, lakini ni muhimu kuwakumbusha kuwa heshima ni nguzo muhimu katika mahusiano ya mataifa. Tunaamini Kenya ina Viongozi wa Dini na Serikali wanaoweza kusaidia katika hili."