Guterres ametoa wito huo katika mkutano na waandishi wa habari kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York na akatoa indhari kwa kusema: "mabilioni ya watu wanakabiliwa na janga la joto kali linalotokana na mawimbi ya joto yanayozidi kukatili maisha huku halijoto ikizidi nyuzi joto 50 kote ulimwenguni. Hiyo ni nyuzi joto 122 Fahrenheit ikiwa ni nusu ya kiwango cha kuchemka”.
Katibu Mkuu wa UN ameendelea kusema: "Ujumbe uko bayana, joto linapanda. Joto kali lina athari kubwa kwa watu na sayari. Ulimwengu lazima ukabiliane na changamoto ya kupanda kwa halijoto.”
Kwa mujibu wa Gutterres, joto linakadiriwa kuua karibu watu nusu milioni kwa mwaka, ikiwa ni takribani mara 30 zaidi ya vifo vinavyosababishwa na vimbunga vya kitropiki.
342/