19 Mei 2025 - 21:46
Mwenyekiti wa JMAT-TAIFA aongoza Kikao cha Maandalizi na Viongozi wa JMAT Kata ya Dar-es-Salaam Kuelekea Kongamano la Qur’an Litakalofanyika Kesho

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- linapenda kuwataarifu wananchi na wadau wote wa amani na maridhiano popote walipo kuwa mapema leo tarehe 19 Mei, 2025, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT-TAIFA), Sheikh Dkt. Alhad Mussa Salum, ameongoza Kikao Maalum na Viongozi wa JMAT kutoka Kata mbalimbali za Jiji la Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa JMAT-TAIFA aongoza Kikao cha Maandalizi na Viongozi wa JMAT Kata ya Dar-es-Salaam Kuelekea Kongamano la Qur’an Litakalofanyika Kesho

Kikao hicho kilichofanyika Makao Makuu ya JMAT-TAIFA kililenga kuweka mikakati na kufanya maandalizi ya mwisho kuelekea Kongamano Kuu la Qur'an litakalofanyika kesho, Mei 20, 2025, katika Ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam.

Kongamano hilo linatarajiwa kuanza saa 8:00 Mchana hadi saa 11:00 Jioni, na litajumuisha washiriki kutoka sehemu mbalimbali za nchi pamoja na wageni maalum kutoka ndani na nje ya Tanzania.

Mwenyekiti wa JMAT-TAIFA aongoza Kikao cha Maandalizi na Viongozi wa JMAT Kata ya Dar-es-Salaam Kuelekea Kongamano la Qur’an Litakalofanyika Kesho

Wito umetolewa kwa wananchi wote, hasa wapenzi wa Qur'an na wadau wa amani, kuhudhuria kwa wingi ili kufanikisha azma ya kueneza mafundisho ya Qur'an na kuimarisha misingi ya maridhiano katika jamii.

Your Comment

You are replying to: .
captcha