2 Julai 2025 - 13:27
Source: Parstoday
Araqchi akosoa kimya cha Baraza la Usalama kuhusu mashambulizi ya Israel dhidi ya Iran

Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekosoa kimya cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia (IAEA) kuhusu mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Iran.

Sayyid Abbas Araqchi na mwenzake wa Misri, Badr Abdelatty, wamzungumza kwa simu na kuchunguza matukio ya kikanda baada ya kusita mashambulizi ya Israel dhidi ya Iran. 

Araqchi ameashiria  hatua ya  jamii ya kimataifa, hasa nchi za Kiislamu na taasisi muhimu za kikanda, ya kulaani vikali uvamizi wa utawala wa Kizayuni dhidi ya Iran na kukosoa kimya cha taasisi mbili muhimu za kimataifa, yaani Baraza la Usalama la UN na wakala wa IAEA, cha kutolaani mashambulizi dhidi ya Iran. 

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran pia amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inafuatilia kwa jadi kutambuliwa pande chokozo na ili kupiwa fidia. 

Katika mazungumzo hayo ya simu, Badr Abdelatty Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri pia amesema amefurahishwa na kusitishwa mashambulizi ya utawala wa Kizayuni na kusisitiza kuwa Misri itaendelea kufanya juhudi za kupunguza hali ya mivutano katika kanda hii ikiwa ni pamoja na usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza. 

342/

Your Comment

You are replying to: .
captcha