Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) – ABNA – Ndege za kivita za Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zilisindikiza ndege iliyokuwa imebeba mwili wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Shahidi Sayyid Ali Hussein Khamenei (ra) aliyeuawa Shahidi pamoja na Mashahidi wa familia yake, muda mfupi kabla ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Shahid Hashemi Nejad mjini Mashhad, Alhamisi tarehe 9 Julai 2026.
Msafara huo wa anga ulifanyika chini ya ulinzi mkali wa jeshi, ukiashiria heshima ya kipekee kwa marehemu na mashahidi wa familia yake. Baada ya kutua, maelfu ya waombolezaji walikuwa wakisubiri kuupokea mwili huo kwa ajili ya kuendelea na shughuli za kuaga na mazishi.
Tukio hilo limeambatana na kaulimbiu "#SimameniKwaAjiliYaMungu" na "#MazishiYaImamuWaWanyonge", huku wananchi kutoka maeneo mbalimbali wakitarajiwa kushiriki katika shughuli za kutoa heshima zao za mwisho kwa mashahidi hao.

Your Comment