Moanyesho ya sanaa ya Kiislamu yanaendelea katika mji wa Lyon nchini Ufaransa. Maonyesho hayo ambayo yalianza tarehe Pili Februari katika Jumba la Makumbusho ya Sanaa mjini Lyon yamepangwa kukamalizika tarehe Nne Julai.
Sanaa kongwe ya Kiislamu ikiwemo ya uchoraji na ufumaji mazulia na kazi nyinginezo za mikono imesababisha mabadiliko makubwa katika nchi za Magharibi kwa kadiri kwamba wasanii mashuhuri wa kazi hizo katika nchi hizo wanachukuliwa kuwa walipata ujuzi wao katika nyanja hizo kutokana na sanaa ya Kiislamu.
Picha za sanaa za kale za ulimwengu wa Kiislamu, yakiwemo mazulia, safari za uvumbuzi katika nchi za Kiislamu na kazi nyinginezo za mikono zinaonyeshwa pia katika maonyesho hayo.