12 Januari 2015 - 17:25
Urusi yaomba mapigano yasitishwe kabla ya mkutano kuhusu amani ya Ukraine

Urusi imetoa wito wa usitishaji mara moja wa uhasama mashariki mwa Ukraine leo na kuonya kwamba serikali ya Ukrane, mjini Kiev inatafuta suluhisho la kijeshi katika mzozo huo.

Urusi  imetoa  wito  wa  usitishaji  mara  moja  wa uhasama mashariki  mwa  Ukraine leo na  kuonya  kwamba  serikali ya Ukrane, mjini  Kiev inatafuta  suluhisho  la  kijeshi  katika  mzozo  huo.

Waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Urusi  Sergei Lavrov  amesema kuwa  juhudi  za  serikali  ya  Ukraine  kutafuta  suluhisho  la  kijeshi katika  mzozo  huo litaleta  madhara  makubwa.

Lavrov  ameongeza  kuwa  usitishaji  kamili  wa  mapigano unapaswa  kufikiwa  haraka  iwezekanavyo  na  kutoa  wito  kwa mataifa  ya  magharibi  kuitolea  mbinyo  kile  alichokieleza  kuwa  ni chama  cha  vita  mjini  Kiev.

Lavrov  anatarajiwa  kukutana  na   wenzake  wa  Ukraine , Ufaransa na  Ujerumani  mjini  Berlin baadaye  leo. Mazungumzo  hayo yanaonekana  kuwa  muhimu  kwa  ajili  ya  mkutano  wa  viongozi wa  nchi  nne  baadaye  wiki  hii  nchini  Kazakhstan.

Tags