-
Ayatollah Ramezani: "Umoja wa Umma wa Kiislamu Ndiyo Njia ya Kukabiliana na Uonevu wa Kimataifa"
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Ulimwengu wa Ahlulbayt (a.s) katika kongamano la "Wanafikra wa Dini; Kubadilishana Uzoefu na Teknolojia Mpya" alisisitiza umuhimu wa umoja wa Kiislamu, uenezi wa pamoja wa mafundisho ya Qur'an na Ahlulbayt (a.s), na utambuzi wa uwezo wa ndani.
-
Kauli ya Sheikh Omar Jane:
Kiongozi wa Jumuiya ya Maulamaa wa Senegal katika Kikao na Katibu Mkuu Jumuiya ya Kimataifa ya AhlulBayt (as):Iran Ipo Ndani ya Nafsi na Maumbile Yetu
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya AhlulBayt (a.s), akiwa katika makao makuu ya Jumuiya ya Maulamaa wa Senegal, amesisitiza juu ya umuhimu wa umoja wa Kiislamu na kuimarisha uwezo wa kielimu na kidini katika ulimwengu wa Kiislamu. Amesema: “Umoja wa Kiislamu Ni Njia ya Kufikia Mamlaka ya Kiulimwengu”
-
Kiongozi wa Baraza la Umoja wa Waislamu wa Pakistan:
Watu wa Gilgit-Baltistan hawatakaa kimya mbele ya dhulma; hata wakikata shingo zetu au kukata ndimi zetu, hatutawahi kumuunga mkono dhalimu
Mwenyekiti wa Baraza la Umoja wa Waislamu wa Pakistan alisisitiza kuwa kusimama dhidi ya dhulma ni jambo lililo katika damu ya watu wa Gilgit-Baltistan, na hakuna nguvu yoyote inayoweza kunyamazisha sauti yao ya kudai haki.
-
JamiatAl-Mustafa S) - Dar es Salaam, inaangazia upande wa Kitaaluma na Kuona Manufaa zaidi katika Mitihani inayofanyika katika Chuo hicho + Picha
Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Mitihani ya mwisho ya muhula wa kwanza kwa mwaka wa masomo wa 2025 imeanza rasmi katika Chuo Kikuu cha Al-Mustafa (S) – Tawi la Dar es Salaam, Tanzania, chini ya mazingira ya kielimu na kiroho yanayojaa bidii na juhudi kubwa kutoka kwa Wanafunzi.
-
Kuanza kwa Mitihani ya Mwisho wa Muhula wa Kwanza wa Mwaka wa Masomo 2025 katika Hawza ya Bibi Zainab (SA), Kigamboni + Picha
Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA- Mitihani ya mwisho wa muhula wa kwanza wa mwaka wa masomo 2025 katika Hawza ya Hazrat Zainab (SA), Kigamboni - Dar-es-Salam, Tanzania, imeanza rasmi. Tunawaombea mafanikio wanafunfi hawa katika mitihani yao, na si tu katika mitihani yao bali pia katika safari yao yote ya kuchuma elimu na maarifa. Kwa ujumla, Mwenyezi Mungu awape ufanisi, maarifa yenye manufaa, na moyo wa kujitahidi kwa ajili ya Uislamu na jamii.
-
China: Marekani ndio chimbuko la ukosefu wa usalama Asia
Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya China imelaani matamshi ya uingiliaji mambo ya Waziri wa Ulinzi wa Marekani kuhusu Bahari ya Kusini ya China na kusisitiza kuwa: "Marekani ikiwa nchi ya kibeberu imekuwa na mchango mkubwa katika kuyumbisha usalama wa Asia.
-
Walowezi zaidi ya 12,000 wavamia msikiti wa al-Aqswa mwezi Mei pekee
Zaidi ya walowezi 12,000 wa Kizayuni wenye misimamo ya kufurutu ada wamevamia msikiti mtakatifu wa al-Aqswa mwezi Mei pekee uliomalizika na kufanya vitendo vya kichochezi katika eneo hilo takatifu.
-
Uwanja wa Ben Gurion wapigwa tena kombora la hypersonic
Jeshi la Yemen limesema kuwa limeanzisha tena operesheni mpya za kulipiza kisasi dhidi ya maeneo yanayolengwa na Israel ndani kabisa ya ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu, ili kukabiliana na jinai na uchokozi unaoendelea dhidi ya Wapalestina wa Gaza.
-
Hamas: Jinai za Israel Gaza zinashinda uhalifu wa Wanazi
Afisa mwandamizi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas amelaani shambulizi la karibuni la Israel dhidi ya wananchi wa Kipalestina wenye njaa waliouawa shahidi wakiendea chakula cha msaada kusini mwa Gaza, akibainisha kwamba mauaji haya yanatuma ujumbe wa wazi kwa ulimwengu wa Kiislamu kwamba wakati umefika wa kusimama dhidi ya wauaji.
-
Yemen yataka makampuni ya kigeni yaondoke 'Israel', mashambulizi yatashadidi
Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen, Mahdi al-Mashat, ametoa onyo kali kwa makampuni ya kigeni yanayowekeza katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu ambazo zimepewa jina bandia la Israel, akibainisha kuwa hatua mpya za kijeshi za Yemen ziko mbioni kuchukuliwa ikiwa uvamizi wa Gaza utaendelea.
-
Jeshi la Anga la Iran liko imara kuilinda nchi kwa nguvu zote
Kamanda wa Jeshi la Anga la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (IRIAF), Brigedia Jenerali Hamid Vahedi amesema kuwa, jeshi hilo liko imara na limejiandaa kikamilifu kulinda anga ya Jamhuri ya Kiislamu kwa hali yoyote ile.
-
Waziri Araghchi yupo Misri kujadili Gaza, uhusiano wa Tehran-Cairo
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi yuko katika mji mkuu wa Misri, Cairo, kwa ajili ya kufanya mazungumzo na maafisa wakuu wa nchi hiyo, juu ya uhusiano wa Jamhuri ya Kiislamu na Misri pamoja na maendeleo katika eneo la Asia Magharibi, yakiwemo mauaji ya kimbari ya Israel huko Gaza.
-
Sera ya vikwazo yakwama, Marekani yasitisha vikwazo vipya dhidi ya Iran
Serikali ya Marekani imesitisha hatua za kuanzisha vikwazo vipya dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, jambo linaloashiria kufeli licha ya kampeni ya vikwazo ya mashinikizo ya juu kabisa ambayo imekuwa ikiendeshwa kwa muda mrefu dhidi ya Iran.
-
Naeem Qassem: Misingi ya Imam Khomeini itaendelea kuwa mwanga wa njia ya mapambano
Sheikh Naeem Qassem, Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon, amesisitiza kuwa mafundisho ya Uislamu asili wa Mtume Muhammad kupitia misingi ya kimapinduzi ya Imam Ruhullah Khomeini (Mwenyezi Mungu Amrehemu) yataendelea kuwa mwanga unaoongoza harakati za mapambano au Muqawama na vuguvugu za ukombozi katika eneo la Asia na ulimwengu mzima wa Kiislamu.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran akutana na Rais wa Misri jijini Cairo
Abbas Araqchi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekutana leo Jumatatu na Rais Abdel Fattah El-Sisi wa Misri jijini Cairo.
-
Ayatollah Ramezani katika Sherehe (Hafla) ya Taklif ya Mabinti wa Senegal: Imani na Elimu ni Mabawa Mawili ya Kuruka (Kupaa) kwa Jamii ya Kiislamu
Kufanyika kwa Sherehe ya Kuvutia ya Taklif (Kufikia umri wa kutekeleza sheria za Kiislamu) kwa Mabinti wa Senegal Huko Dakar sambamba na uwepo wa Ayatollah Reza Ramezani
-
Ayatollah Ramezani Mjini Dakar: Mafundisho ya Ahlul-Bayt (a.s) ni Njia ya Kumfikia Mungu
Katika majlisi ya maombolezo ya kuadhimisha shahada ya Imamu Jawad (a.s) iliyofanyika katika mji mkuu wa Senegal, Dakar, Ayatollah Reza Ramadhani — Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt (a.s) — alisisitiza: "Kufaidika na mafundisho na maneno ya Ahlul Bayt (a.s) hutusaidia katika safari ya kimatendo ya kumkaribia Mwenyezi Mungu." Amebainisha kuwa: "Maudhui yanayotolewa na Ahlul Bayt (a.s) ni ya ki-Tawhidi, yamejengwa juu ya msingi wa maumbile ya mwanadamu (fitra), na yanakubaliana kikamilifu na akili ya binadamu."
-
Ayatollah Ramezani Awasili Nchini Senegal na Kupoklewa na Viongozi wa Kidini wa Nchi Hiyo+ Picha
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt (a.s) azuru Senegal kwa mwaliko wa viongozi wa kidini.
-
Habari Pichani| Mkutano wa "Nafasi ya Wanazuoni wa Kiislamu katika Mabadiliko ya Dunia kwa Msingi wa Kesi ya Palestina" katika Mji Mkuu wa Senegal
Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul Bayt (a.s) — ABNA, mkutano uliohusu "Nafasi ya Wanazuoni wa Kiislamu katika Mabadiliko ya Dunia kwa mtazamo wa Palestina na ufafanuzi wa mpango wa Kiongozi wa Mapinduzi kuhusu mustakbali wa Palestina" umefanyika katika mji mkuu wa Senegal, Dakar.