Matembezi ya Amani
-
Siku ya Quds Duniani:
Mojawapo ya sehemu ya malengo ya Siku ya Quds Duniani, ni kuienzi Amani ya Dunia nzima
Mojawapo ya sehemu ya malengo ya Siku ya Quds Duniani, ni kuienzi na kuidumisha Amani ya Dunia nzima. Waislamu waishi kwa Amani, Wakristo waishi kwa Amani, na hata Mayahudi waishi kwa Amani, na mtu yeyote asionewe na kudhulumiwa popote pale alipo Duniani.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Maandamano ya Mwaka huu yatakuwa miongoni mwa Maandamano yenye Heshima Kubwa katika Siku ya Quds
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: Mwenyezi Mungu akipenda (Insha Allah), Matembezi (Maandamano) ya Mwaka huu yatakuwa miongoni mwa Matembezi bora zaidi, Matukufu na yenye Heshima Kubwa katika Siku ya Quds.
-
Mwaliko (Wito) wa Ayatollah Ramadhani kwa watu wa Gilan Kushiriki Katika Maandamano ya Siku ya Quds ya 2025
Ayatollah "Reza Ramezani", Mwakilishi wa Wananchi wa Gilan katika Baraza la Wataalamu wa Uongozi, katika Mkesha wa Siku ya Quds Duniani, amewaalika na kuwahimiza watu kushiriki katika Maandamano ya Siku hii.
-
Hazrat Ayatollah Javadi Amoli:
Siku ya Quds ni sehemu ya "Siku ya Kimataifa ya Uislamu"
Ayatollah Javadi Amoli, akiwaalika watu kushiriki katika Maandamano ya Siku ya Quds, alisema: Ni wajibu wetu sote kushiriki katika Maandamano haya, kwanza, Na kila mmoja wetu kwa mujibu wa elimu tuliyo nayo, awe na nia ya Tawalli na Tabarri ya Kimungu, pili, na kujaribu kufayanya kuwa maandamano mapana zaidi, tatu, yaani tuyafanye maandamano haya kwa nia ya kuwa karibu na kuwaheshimu na kuwathamini Mashahidi wa njia hii, ili hatua hizi zote zithibitishwe na Dhati Takatifu ya Mwenyezi Mungu.
-
Siku ya Quds Duniani:
Amani ya Palestina, ni Amani ya Tanzania
Wito wa kujitokeza kwa watu wote, Waislamu na Watanzania wote wapenda Haki katika siku ya Kimataifa ya Quds, ili kuungana na Wapalestina katika kutetea Haki zao za Kibinadamu katika Taifa lao la Palestina, na vile yakiwa ni Matembezi ya Masjid Al_Aqsa, ambayo ni Kibla cha Kwanza cha Waislamu.
-
Jumuiya ya walimu wa Seminari ya Qom:
Wananchi wa Iran wanapaswa kutangaza utayarifu wao wa kuwasaidia wapiganaji wa Palestina kwa kushiriki katika maandamano ya Siku ya Quds
Katika kizingiti cha Siku ya Quds Duniani, Jumuiya ya Walimu wa Seminari ya Qom imetoa taarifa ikizitaka sehemu zote za Taifa pendwa la Iran kushiriki kikamilifu katika Matembezi ya Amani ya Siku hii ya Quds na kutangaza kwa mara nyingine uungaji mkono wao kwa Muqawamah (Upinzani) wa Kiislamu wa Palestina.