mafunzo
-
Maulana Sheikh Hemed Jalala Atoa Mafunzo Matano Muhimu Kutokana na Mazishi ya Sayyid Ali Khamenei
Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Shia Tanzania (TIC), Maulana Sheikh Hemed Jalala Mwakindenge, amesisitiza umuhimu wa umoja wa Mashia, Waislamu na watu wa dini mbalimbali, pamoja na uzalendo na kuheshimu viongozi wanaolitumikia taifa na jamii kwa uadilifu.
-
Kamanda wa Makao Makuu ya Pamoja ya Ulinzi wa Anga ya Iran: Kusasisha Uwezo na Mafunzo ni Lazima ili Kukabiliana na Maendeleo Mapya
Kamanda wa Makao Makuu ya Pamoja ya Ulinzi wa Anga nchini Iran, Brigedia Jenerali Alireza Elhami, amesema kusasisha vifaa, uwezo na mitaala ya mafunzo ni jambo la lazima ili kukabiliana na mabadiliko ya vitisho vya anga na maendeleo ya teknolojia za kijeshi.
-
Chuo cha Kiislamu cha Wafuasi wa Ahlul-Bayt (a.s) Chafanya Majlisi ya Maombolezo ya Muharram - Dar es Salaam
Jamiatul Mustafa International Foundation - Chuo cha Kiislamu cha Wafuasi wa Ahlul-Bayt (a.s.) jijini Dar es Salaam kimefanya majlisi ya maombolezo ya Muharram, ambapo mhadhiri alikuwa Dkt. Reihan Yasin.
-
Katika Ugeni wetu kwa Mwenyezi Mungu, tuvae “Vazi Halisi na Bora Zaidi” la Ucha Mungu!
Katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, ambao ni karamu ya Mwenyezi Mungu, “brand” ya kweli si mavazi ya gharama bali ni taqwa, ikhlasi, subira na maadili mema. Hivi ndivyo vinavyomfanya mja awe mrembo mbele ya Mwenyezi Mungu na kufuzu katika meza ya rehema na maghfira.
-
Mufti Mkuu wa Tanzania:
"Qur’an Tukufu Inahimiza Amani Kama Msingi wa Maisha ya Mwanadamu | Tunajifunza Amani Kutoka Katika Kisa cha Nabii Ibrahim (as)
Katika kufafanua hoja yake, Mufti Mkuu wa Tanzania ametaja kisa cha wageni wa Nabii Ibrahim (as) kama kinavyosimuliwa ndani ya Qur’an Tukufu. Amesema kuwa wageni hao walipoingia nyumbani kwa Nabii Ibrahim (as), walimpa maamkizi ya amani, naye akajibu kwa maamkizi yale yale ya amani.
-
Darsa za Kielimu na Maarifa | Mafunzo ya Ahlul-Bayt (a.s) Yaendelea kuwaangazia Waumini Kila Alhamisi Mjini Moshi +Picha
Kupitia mihadhara hii, waumini hupata fursa ya kujifunza misingi ya itikadi, maadili ya Kiislamu, na mwongozo wa maisha unaojengwa juu ya haki, uadilifu na kumcha Mwenyezi Mungu.
-
Riwaya ya Mapambano ya Wapalestina Dhidi ya Ukoloni katika Miaka ya 1930 / Mizizi ya Uhalifu na Unyama wa Kizayuni Leo Iko Wapi?!
Filamu Palestine 36 inaonyesha kwa ustadi mkubwa kwamba uhalifu wa utawala wa Kizayuni unatokana moja kwa moja na ukatili, uvamizi na unyama wa Dola ya Uingereza katika kipindi cha ukoloni.
-
Mafunzo kutoka katika Maisha ya Bibi Fatima Zahra (a.s) kwa Ajili ya Kujenga Utulivu katika Familia +
Hadithi ya Mgawanyo wa Majukumu kati ya Imam Ali (a.s) na Bibi Fatima Zahra (s.a) Hadithi inayosimulia jinsi Mtume Mtukufu (s.a.w.w) alivyogawa majukumu ya kifamilia kati ya Imam Ali (a.s) na Bibi Fatima (a.s) ni mfano wa hekima katika ujenzi wa familia ya Kiislamu.
-
Burkina Faso: Daktari Aliyemkosoa Rais Traoré Atumwa Vitani kupambana na Magaidi Baada ya kupata Mafunzo ya Kijeshi - Kisa Kinachozua Mjadala Mpana
Rais Ibrahim Traoré, akizungumza katika mahojiano ya televisheni ya kitaifa, alithibitisha tukio hilo na kusema kwa maneno makali: “Kama kuna daktari, mwalimu, au mfanyabiashara anayehisi anajua zaidi kuhusu vita kuliko wanajeshi wetu, basi ni bora naye achangie kwa vitendo - aende vitani.”
-
Mtume Mtukufu (s.a.w.w) na Sanaa ya Kuonyesha Mapenzi Ndani ya Familia
Familia katika mtazamo wa Mtume Mtukufu (s.a.w) si tu kitovu cha utulivu, bali ni uwanja wa kudhihirika kwa maadili ya kimungu. Yeye (s.a.w.w), kwa tabia yake tukufu na kwa kushikamana na mafundisho ya Qur'an kama vile: " - Semeni naye - kwa upole" (قَوْلًا لَّیِّنًا), na "Hakika wewe ni mwenye tabia njema kabisa" (إِنَّکَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِیمٍ), alionesha ustadi wa kipekee katika kuonyesha mapenzi kwa wake na watoto wake. Makala hii, ikitegemea vyanzo vya Kishia, inachunguza mwonekano wa upendo wa Mtume (s.a.w.w) ndani ya familia, na inatoa mafunzo ya kudumu kwa familia za leo.
-
Kozi zenye Mada Maalum | “Misingi ya Itifaki na Ustaarabu”, "Dhana, Historia, Dira, Dhima na Hadhi ya JMAT", Na Zingine Zitatolewa kupitia JMAT
Lengo kuu la kozi hizi ni kuwajengea washiriki uwezo wa kuwa mabalozi wa maadili, ustaarabu na mawasiliano bora katika jamii na katika nafasi zao za kazi au uongozi.
-
JMAT Yatangaza Mafunzo ya Msingi ya Itifaki na Ustaarabu (J-PEC) Jijini Dar es Salaam
Taarifa zinaeleza kuwa, mafunzo hayo yatafanyika kuanzia tarehe 16 – 18 Septemba 2025, katika Ukumbi wa Nefaland Hotel Hall, Manzese – Argentina, Dar es Salaam, kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 11:00 jioni kila siku.