uingereza
-
Ufichuzi Mpya wa Siri Huko Uingereza: Vikosi Maalum Vilifyatua Risasi na Kuua Watoto Waafghani Wakiwa Wamelala Kitandani
Maafisa wa jeshi nchini Uingereza wamekiri kuhusika katika mauaji ya watoto nchini Afghanistan na kusisitiza kuwa: mauaji hayo ya nje ya mfumo wa sheria yalitekelezwa, na huenda haya ni sehemu ndogo tu ya kile kilichotokea!
-
Kuendelea kwa Mjadala Mkali Kuhusu Mbio ya Hisani ya Msikiti wa East London; Wito Watolewa kwa Mapitio ya Sera ya Utenganisho wa Jinsia
Baada ya mashambulizi makubwa ya vyombo vya habari vya Uingereza dhidi ya mbio ya hisani iliyoandaliwa na Msikiti wa East London kwa sababu ya utenganishaji wa kijinsia, Tume ya Usawa na Haki za Kibinadamu ya Uingereza imeitangaza kwamba waandaaji wa tukio hilo wamekubali kupitia upya sera zake kabla ya awamu ijayo ya mashindano. Hata hivyo, msikiti huo umeeleza kwamba matukio kama hayo yapo kwa wingi katika maeneo mbalimbali ya Uingereza-ikiwemo mashindano maalumu ya wanawake na vipindi vya kuogelea vinavyoandaliwa katika vituo vya jamii ya Kiyahudi-lakini hakuna hata moja kati ya matukio hayo yaliyowahi kusababisha mjadala au msukosuko kama huu.
-
Barua ya Iran, Urusi na China kwa Grossi: Wajibu wa Kuripoti wa IAEA Umefikia Mwisho
Wawakilishi wa kudumu wa Iran, Urusi na China katika Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) wamemwandikia barua rasmi Rafael Grossi, Mkurugenzi Mkuu wa wakala huo, wakisisitiza kuwa kwa kumalizika kwa muda wa utekelezaji wa Azimio la 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, jukumu la IAEA la kuwasilisha ripoti chini ya azimio hilo limefikia mwisho, na kwamba hatua yoyote mpya katika mwelekeo huo haina uhalali wa kisheria.
-
Watu 2 wameuawa katika shambulio la silaha mbele ya sinagogi ya Kiyahudi huko Manchester, Uingereza
Tukio lililotokea sambamba na sherehe ya Yom Kippur mbele ya sinagogi ya Kiyahudi huko Manchester, Uingereza, limesababisha vifo vya watu 2 na kujeruhi wengine 3.
-
Hasira ya Viongozi wa Kizayuni Kufuatia Hatua ya Uingereza, Australia na Canada Kutambua Nchi ya Palestina
Hatua ya nchi tatu — Uingereza, Australia na Canada — kutambua rasmi nchi huru ya Palestina, imeibua hasira na ghadhabu kubwa miongoni mwa viongozi wa utawala wa Kizayuni.
-
Baghdad yamuita Balozi wa Uingereza kufuatia matamshi yake kuhusu Hashd al-Shaabi
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iraq imemuita balozi wa Uingereza mjini Baghdad kutokana na matamshi yake kuhusu nafasi ya Hashd al-Shaabi katika mfumo wa usalama wa Iraq, na imeonyesha majibu makali juu ya kauli hizo.
-
Funzo Kuu la Arbaeen ni Msimamo Imara, Subira, na Mapambano: Ayatollah Ramazani
Mkutano wa awali wa wavuti (webinar) ulioandaliwa na Idara ya Masuala ya Kimataifa ya Jumuiya ya Kimataifa ya AhlulBayt (a.s.) kuhusu mada “Kutathmini Ujumbe wa Kimataifa wa Arbaeen ya Imam Hussain (a.s): Kutoka Wilayat hadi Wajibu” umefanyika.
-
Waziri Mkuu wa Uingereza ametuma salamu za pongezi kwa Waislamu kwa mnasaba wa Sikukuu ya Eid al-Adha
Baadhi ya viongozi wa kisiasa wa Uingereza, wakiwemo Waziri Mkuu wa nchi hiyo, wametuma salamu za pongezi kwa Waislamu wa Uingereza na ulimwenguni kote kwa mnasaba wa Sikukuu ya Eid al-Adha.
-
Mazungumzo ya Biashara Huria kati ya Uingereza na Israeli yameghairiwa (yamesitishwa); Balozi wa Israeli London aitwa
Serikali ya Uingereza imeamua kusitisha mazungumzo ya mkataba wa biashara huria na utawala wa Kizayuni kutokana na kuongezeka kwa ghasia zinazofanywa na wakazi wa maeneo ya mizozo na uendeshaji wa operesheni za kijeshi katika ukanda wa Ghaza. Aidha, imeweka vikwazo dhidi ya watu na mashirika yanayohusiana na ghasia hizi. Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza pia amemwita balozi wa utawala huo ili kutoa maelezo kuhusu hali hiyo na kusisitiza umuhimu wa kuacha mara moja matendo ya ukatili.
-
Onyo la Baraza la Wawakilishi la Yemen: Vikosi vya jeshi vitajibu ipasavyo
Baraza la Wawakilishi la Yemen limetoa taarifa likionya kuhusu matokeo ya hujuma za Marekani na Uingereza dhidi ya raia wa nchi hii.