23 Februari 2016 - 19:13
Obama aandaa mipango kulifunga gereza la Guantanamo

Rais Barack Obama anatarajiwa leo kutoa msukumo wa mwisho kuhusu kulifunga gereza lenye utata la Marekani la Guantanamo Bay

Shirika la habari la ABNA linaripoti kuwa: Rais  Barack Obama  anatarajiwa  leo  kutoa  msukumo  wa mwisho kuhusu  kulifunga  gereza lenye  utata  la Marekani  la  Guantanamo Bay, akiwa  na  matumaini  ya kutimiza ahadi  aliyotoa  wakati  wa  kampeni ya  uchaguzi.

Ikiwa  ni  mwaka  mmoja  tu  kabla  ya  kuacha  madaraka, Obama  ataweka  wazi  nafasi  za  kulifunga  gereza  hilo katika  taarifa  atakayoitoa  leo.

Kiasi  ya  wafungwa  90  watuhumiwa  wa  ugaidi bado wako  katika  gereza  hilo  la  Guantanamo , ambalo linauwezo  wa  kuwahifadhi  wafungwa  700  na  limekuwa eneo  linalotambulika  duniani  kote  kama eneo  la mateso, kifungo  bila kufikishwa  mahakamani  pamoja  na mavazi  yake  ya  rangi  ya  chungwa.

Kwa  miaka  kadhaa, juhudi  za  Obama  kulifunga  gereza hilo zimezuiwa  na  wabunge  wa  chama  cha  Republican, wengi  wao  wanaliona  kuwa  ni  chombo  chenye manufaa  katika  kupambana  na  ugaidi.

Mwisho wa habari/ 291