Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA- Licha ya mashambulizi makubwa ya anga na mabomu ya jeshi la Israel kusini mwa Lebanon, watu walihudhuria uchaguzi wa mitaa kwa wingi na ari kubwa. Wapiga kura wengi walikuwa wafuasi wa upinzani (Muqawamah) na makundi yanayohusiana na Hizbullah na Harakati ya Amal, wakionyesha tena msaada wao wa kisiasa kwa chaguo la upinzani (Muqawamah) kupitia ushiriki wao.
Katika vijiji vingi, kutokana na makubaliano ya kisiasa, orodha za wagombea zilijitokeza bila ushindani, na hata katika maeneo yaliobaki, Hizbullah na washirika wake (walishinda kwa) wingi. Mashambulizi ya anga yaliyoongezeka katika siku za mwisho kabla ya uchaguzi yalihamasisha watu zaidi kushiriki badala ya kuwatisha.
Jeshi la Lebanon na vyombo vya usalama, pamoja na waangalizi wa uchaguzi kutoka maeneo mbalimbali, walifanya juhudi kuhakikisha usalama wa uchaguzi na mchakato wa kupiga kura unafanyika kama ilivyopangwa.
Mashindano makali yalikuwepo zaidi katika miji ya Sour na Nabatiyeh, ambapo orodha mbili za wagombea huru zilipigana (zilishindana) na zile zinazohusiana na Amal na Hizbullah. Kwa ujumla, uchaguzi huo ulionyesha msaada mkubwa (sapoti kubwa) ya watu wa kusini mwa Lebanon kwa Upinzani (Muqawamah) dhidi ya uvamizi wa Israel.
Your Comment