Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA- Katika mwendelezo wa kuadhimisha siku hizi za Ashu'ra juu ya Kifo cha Kishahidi cha Mjukuu wa Mtukufu Mtume wetu Muhammad (saww), Al-Imam Hussein (as), Taasisi ya Desk and Chair Foundation ya Jijini Mwanza chini ya Mwenyekiti wake Alhajj, Dokta Sibtain Megji imemkabidhi Viti mwendo 20 Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Seketoure , kwa ajili ya matumizi ya hospitali hiyo kwa wagonjwa wenye uhitaji.






Your Comment