Kwa mujibu wa shirika la habari la ABNA likinukuu shirika la habari la serikali ya Syria (SANA), taarifa hiyo ilisema: "Katika mfumo wa juhudi zinazoendelea za kupambana na ugaidi, habari zilipatikana kuhusu nia ya kundi hili kufanya operesheni za kujitolea mhanga na mashambulizi dhidi ya makanisa na maeneo ya mikusanyiko ya raia wakati wa sherehe za mwaka mpya."
Wizara hiyo ilisema kuwa katika hatua ya kuzuia, afisa wa usalama kwenye kizuizi katika eneo la Bab al-Faraj huko Aleppo alimshuku mtu mmoja. Gaidi huyo alifyatua risasi na kumuua afisa huyo, kisha akajilipua na kuwajeruhi maafisa wengine wawili waliokuwa wakijaribu kumkamata.
Your Comment