2 Januari 2026 - 15:55
Source: ABNA
Madai ya utawala wa Julani kuhusu kuzima mpango wa Daesh wa kushambulia sherehe za Mwaka Mpya

Wizara ya mambo ya ndani ya utawala wa Julani imetangaza kuwa imezima mpango wa kundi la kigaidi la Daesh (ISIS) wa kushambulia sherehe za kuanza kwa mwaka mpya katika mikoa kadhaa ya Syria, haswa mji wa Aleppo.

Kwa mujibu wa shirika la habari la ABNA likinukuu shirika la habari la serikali ya Syria (SANA), taarifa hiyo ilisema: "Katika mfumo wa juhudi zinazoendelea za kupambana na ugaidi, habari zilipatikana kuhusu nia ya kundi hili kufanya operesheni za kujitolea mhanga na mashambulizi dhidi ya makanisa na maeneo ya mikusanyiko ya raia wakati wa sherehe za mwaka mpya."

Wizara hiyo ilisema kuwa katika hatua ya kuzuia, afisa wa usalama kwenye kizuizi katika eneo la Bab al-Faraj huko Aleppo alimshuku mtu mmoja. Gaidi huyo alifyatua risasi na kumuua afisa huyo, kisha akajilipua na kuwajeruhi maafisa wengine wawili waliokuwa wakijaribu kumkamata.

Your Comment

You are replying to: .
captcha