Kwa mujibu wa shirika la habari la Abna, Abdolreza Rahmani Fazli kwenye ukurasa wake wa kibinafsi katika mtandao wa kijamii aliandika: Mapatano yoyote yanayowezekana lazima yaambatane na dhamana ya mataifa makubwa na pia yawe mbele ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. China na Urusi ni mataifa mawili makubwa na yenye ushawishi, na kwa kuzingatia nafasi ambayo China anayo kwa Iran na nchi nyingine za eneo la Ghuba ya Uajemi, Beijing inaweza kuwa mdhamini wa mapatano yoyote.
Balozi wa Iran nchini China alisema: Mapatano yoyote yanayowezekana lazima yawe na dhamana ya mataifa makubwa.
Your Comment