Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Sayyid Abbas Araghchi, amefanya mkutano na ujumbe wa Fronti ya Umma ya Ukombozi wa Palestina (PFLP) kwa lengo la kujadili hali ya Palestina na hatua za kuimarisha mshikamano wa harakati za muqawama.

Katika mkutano huo, pande hizo zilisisitiza umuhimu wa kuendelea kuunga mkono wananchi wa Palestina na kusimama dhidi ya sera za uvamizi, ukandamizaji na uhalifu unaofanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya watu wa Gaza na maeneo mengine ya Palestina.
Mkutano huo pia umeonyesha msimamo thabiti wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wa kuendelea kuiunga mkono kadhia ya Palestina na harakati za ukombozi, sambamba na kuimarisha umoja wa makundi ya muqawama katika kukabiliana na changamoto zinazolikabili eneo la Mashariki ya Kati.

Your Comment