Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– maelfu ya waumini na waombolezaji wameendelea kumiminika katika Msala wa Imam Khomeini (Quds Sirruh) mjini Tehran kushiriki katika marasimu ya kuuaga mwili mtukufu wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Imam Sayyid Ali Khamenei (Qudsallahu Nafsahu Az-Zakiyyah).
Picha hizi zinaonyesha umati mkubwa wa wananchi ukitoa heshima za mwisho mbele ya mwili mtukufu wa Kiongozi Shahidi, huku hali ya majonzi, dua na uaminifu kwa misingi ya Mapinduzi ya Kiislamu ikitawala katika ukumbi mzima wa marasimu.
Marasimu hayo yamehudhuriwa pia na viongozi wa ndani na wa kimataifa, wanazuoni wa dini pamoja na ujumbe kutoka mataifa mbalimbali, wakisisitiza mshikamano wao na wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kipindi hiki cha maombolezo.
Your Comment