China
-
Marekani yaonya China au Urusi huenda wanasaidia Iran kushambulia malengo ya Marekani
Maafisa wa Marekani wana wasiwasi kuwa China au Urusi huenda wanatoa msaada kwa Iran katika mashambulizi yake dhidi ya malengo ya Marekani, kwa mujibu wa ripoti ya Wall Street Journal. Ripoti hiyo pia inasema Iran sasa inatumia makombora yanayoweza kuendeshwa wakati wa kuruka na yanayosafiri kwa kasi kubwa sana, jambo linalofanya ulinzi wa anga kuwa mgumu zaidi. Hatua hiyo imeongeza hofu kuhusu uwezo wa Iran wa kupenya mifumo ya ulinzi na kuongeza hatari ya mzozo mpana zaidi katika eneo hilo.
-
Ghalibaf: Kuimarisha uhusiano wa kimkakati kati ya Iran na China ni lazima
Rais wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha uhusiano wa kimkakati, kisiasa na kibunge kati ya Iran na China, akibainisha kuwa mabadiliko ya hivi karibuni ya kikanda na kimataifa yameufanya ushirikiano wa karibu kati ya Tehran na Beijing kuwa wa lazima zaidi kuliko wakati wowote.
-
Uchambuzi: Kinachoendelea kati ya Iran na Marekani; Makubaliano au Mkakati wa Kusubiri?
Kwa mujibu wa hali halisi ilivyo, kikwazo kikubwa katika mazungumzo kati ya Iran na Marekani si kufikia makubaliano, bali ni ukosefu wa uaminifu na dhamana ya utekelezaji wake. Tehran inasisitiza kuwa haitasaini makubaliano yoyote kwa shinikizo la Washington, bali yale yatakayolinda maslahi yake na usalama wa eneo.
-
Iran, China na Urusi katika Baraza la Magavana la IAEA: Rasimu ya Azimio dhidi ya Iran ni ya Kisiasa na Haina Tija
Iran, China na Urusi zimekosoa rasimu ya azimio dhidi ya Iran katika Baraza la Magavana la IAEA, zikisema ni ya kisiasa na inalenga kuongeza shinikizo badala ya kuimarisha ushirikiano wa kimataifa, huku zikisisitiza kuwa hatua hizo zinaweza kuhatarisha diplomasia na utulivu wa nyuklia.
-
Shirika la Ushirikiano la Shanghai Latangaza Msimamo wa Kuliunga Mkono Iran Dhidi ya Uvamizi wa Kizayuni na Marekani
🔹 Waziri wa Mambo ya Ndani wa Iran, Eskandar Momeni, amesema kuwa nchi zote wanachama wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai, hususan China na Russia, zimeonyesha kuunga mkono Iran katika kukabiliana na kile kinachoitwa uvamizi wa Kizayuni na Marekani, huku zikichukua misimamo chanya kuhusu suala hilo.
-
Trump Adai Marekani na China Zina Uwezo wa Kushughulikia Urani Iliyoboreshwa ya Iran
Rais wa Marekani Donald Trump amedai kuwa nyenzo za urani iliyoboreshwa za Iran zilizohifadhiwa chini ya ardhi zinaweza kutolewa na kushughulikiwa kwa uratibu wa Iran na IAEA, jambo lililozua mjadala mpya kuhusu mustakabali wa mpango wa nyuklia wa Tehran
-
Dai la Wall Street Journal: Vikosi vya Marekani Vavamia Meli Iliyokuwa Ikisafirisha Shehena ya China Kwenda Iran
Kwa mujibu wa madai ya gazeti la Wall Street Journal, vikosi maalum vya Marekani vilivamia na kuteka meli iliyokuwa ikibeba shewena ya kijeshi kutoka China kuelekea Iran katika Bahari ya Hindi mnamo Novemba 2025.
-
Makampuni makubwa ya silaha kutoka Russia, Marekani, China na Ulaya waanza kunakili teknolojia ya Droni "Shahed“ ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Umaarufu unaozidi kuongezeka wa drone ya Shahed ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran umeleta mabadiliko makubwa katika fikra za kiulinzi duniani, na sasa mataifa yenye uwezo mkubwa yanaanza kujifunza kutoka kwa taifa lililotumia ubunifu na uhalisia badala ya gharama kubwa.
-
Mkutano wa Balozi wa China mjini Kabul na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Taliban kuhusu vifo vya raia wa China mpakani mwa Afghanistan na Tajikistan
“Balozi wa China mjini Kabul, katika mkutano na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Taliban, alitaja mashambulio ya hivi karibuni dhidi ya wafanyakazi wa China katika eneo la mpakani kati ya Tajikistan na Afghanistan — ambayo yamesababisha vifo vya watu 5 na kuwajeruhi wengine kadhaa — kuwa ‘kitendo cha maadui kwa ajili ya kuleta kutokuaminiana’. Pia aliishukuru Taliban kwa kuanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo.
-
Barua ya Iran, Urusi na China kwa Grossi: Wajibu wa Kuripoti wa IAEA Umefikia Mwisho
Wawakilishi wa kudumu wa Iran, Urusi na China katika Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) wamemwandikia barua rasmi Rafael Grossi, Mkurugenzi Mkuu wa wakala huo, wakisisitiza kuwa kwa kumalizika kwa muda wa utekelezaji wa Azimio la 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, jukumu la IAEA la kuwasilisha ripoti chini ya azimio hilo limefikia mwisho, na kwamba hatua yoyote mpya katika mwelekeo huo haina uhalali wa kisheria.
-
Makabiliano ya kimya kati ya Misri na Israel huko Sinai
Kuongezeka kwa uwepo wa kijeshi wa Misri katika Sinai na ushirikiano wa kimkakati na China, kumeanzisha mgogoro mpya kati ya Cairo na Tel Aviv na kuweka hatarini mustakabali wa mkataba wa amani wa Camp David.
-
China Yaonesha Nguvu za Kijeshi Katika Gwaride Huku Rais wa China Xi Akisimama Pamoja na Rais Putin na Rais Kim +Picha
China iliandaa gwaride kubwa la kijeshi kuonesha uwezo wake wa kivita, huku Rais Xi Jinping akisalimiana na kusimama pamoja na Rais Vladimir Putin wa Urusi na Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un. Hafla hiyo iliangazia umoja wa kisiasa kati ya mataifa hayo na kuonesha silaha mpya na teknolojia ya kisasa ya kijeshi mbele ya maelfu ya watazamaji na viongozi wa kimataifa.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ataka Utekelezaji wa Makubaliano ya Kistratejia kati ya Iran na China
Ayatollah Khamenei amesisitiza nafasi ya kihistoria na ya kimkakati ya Iran na China katika bara la Asia na duniani, na akasema kuwa: "Iran na China, zikiwa na historia ya ustaarabu wa kale katika pande mbili za Asia, zina uwezo wa kuleta mabadiliko katika medani ya kimataifa na kikanda. Kuweka katika vitendo vipengele vyote vya makubaliano ya kistratejia, kutarahisisha njia hii."
-
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa China na Pakistan Wawasili Kabul, Afghanistan
Waziri wa Mambo ya Nje wa China alipokelewa na Amir Khan Muttaqi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Kaimu ya Afghanistan, na kufanya naye mazungumzo. Wakati huo huo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Pakistan alipokelewa na Hanafi Wardak, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Taliban.
-
Wanasayansi wa China Watengeneza Bomu Jipya Lenye Nguvu Bila Mionzi ya Nyuklia
Habari njema ni kuwa, kwa kuwa bomu hili si la nyuklia, halitoi mionzi yoyote hatari ya sumaku au ya miale ya nyuklia. Teknolojia hii mpya inaweza kubadilisha matumizi ya silaha za nguvu zisizo za nyuklia katika siku zijazo.