Shirika la habari la serikali ya China Xinhua, limeripoti kuwa serikali ya nchi hiyo imewakamata zaidi ya watu 30,000 wakati wa msako wa miezi miwili dhidi ya picha za uchi na kamari.
Rais wa China Xi Jinping amesema amefanya mazungumzo yenye tija na Rais wa Marekani Barack Obama na nchi hizo mbili zimekubaliana kuharakisha mazungumzo kuhusu uwekezaji wa pamoja na kuboresha uhusiano wa kijeshi.
Viongozi wa China na Japan wamefanya mkutano wa nadra baina yao hii leo baada ya miaka miwili ya uhasama kati ya nchi zao. Mazungumzo yao yanafanyika pembezoni mwa mkutano wa kilele wa nchi za Asia na Pacifiki APEC.