Siku ya Quds
-
Siku ya Quds Duniani:
Kongamano la Siku ya Quds Duniani lilifanyika Jijini Tanga, Tanzania
Kuna umuhimu Mkubwa kwa Waislamu na Watu wote huru na wapenda Haki Duniani, kuzidi kusimama pamoja na wadhulumiwa wa Palestina na kutetea Haki za watu wote wanyonge popote pale walipo Duniani. Watu mbalimbali kutoka Jiji la Tanga walihudhuria katika Mkusanyiko huu wa kuhuisha Siku ya Kimataifa ya Quds, wakiwemo Viongozi wa Taasisi mbalimbali za Kidini na Madhehebu mbalimbali.
-
Takriban watu 20 Wameuawa baada Wanajeshi wa Nigeria kushambulia Maandamano ya Siku ya Quds Mjini Abuja
Makumi ya waandamanaji wanaounga mkono Palestina wameuawa na kujeruhiwa baada ya vikosi vya usalama kuwafyatulia risasi wakiwa kwenye Maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds katika Mji Mkuu wa Nigeria.
-
Kulaani Ukandamizaji na Mauaji ya watu wa Nigeria Katika Siku ya Al-Quds | Moto wa Mwamko wa Kiislamu Hautazimika
Baraza la Uratibu wa Tabligh za Kiislamu, limelaani ukandamizaji wa Maandamano ya Siku ya Quds Duniani nchini Nigeria, na limetangaza kuwa: Jinai hizo za kipofu zitazidisha azma ya Mataifa ya Kiislamu kukabiliana ipasavyo na mfumo wa ukoloni na uistikbari.
-
Siku ya Quds Duniani:
Mojawapo ya sehemu ya malengo ya Siku ya Quds Duniani, ni kuienzi Amani ya Dunia nzima
Mojawapo ya sehemu ya malengo ya Siku ya Quds Duniani, ni kuienzi na kuidumisha Amani ya Dunia nzima. Waislamu waishi kwa Amani, Wakristo waishi kwa Amani, na hata Mayahudi waishi kwa Amani, na mtu yeyote asionewe na kudhulumiwa popote pale alipo Duniani.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Maandamano ya Mwaka huu yatakuwa miongoni mwa Maandamano yenye Heshima Kubwa katika Siku ya Quds
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: Mwenyezi Mungu akipenda (Insha Allah), Matembezi (Maandamano) ya Mwaka huu yatakuwa miongoni mwa Matembezi bora zaidi, Matukufu na yenye Heshima Kubwa katika Siku ya Quds.
-
Mwaliko (Wito) wa Ayatollah Ramadhani kwa watu wa Gilan Kushiriki Katika Maandamano ya Siku ya Quds ya 2025
Ayatollah "Reza Ramezani", Mwakilishi wa Wananchi wa Gilan katika Baraza la Wataalamu wa Uongozi, katika Mkesha wa Siku ya Quds Duniani, amewaalika na kuwahimiza watu kushiriki katika Maandamano ya Siku hii.
-
Hazrat Ayatollah Javadi Amoli:
Siku ya Quds ni sehemu ya "Siku ya Kimataifa ya Uislamu"
Ayatollah Javadi Amoli, akiwaalika watu kushiriki katika Maandamano ya Siku ya Quds, alisema: Ni wajibu wetu sote kushiriki katika Maandamano haya, kwanza, Na kila mmoja wetu kwa mujibu wa elimu tuliyo nayo, awe na nia ya Tawalli na Tabarri ya Kimungu, pili, na kujaribu kufayanya kuwa maandamano mapana zaidi, tatu, yaani tuyafanye maandamano haya kwa nia ya kuwa karibu na kuwaheshimu na kuwathamini Mashahidi wa njia hii, ili hatua hizi zote zithibitishwe na Dhati Takatifu ya Mwenyezi Mungu.
-
Siku ya Quds Duniani:
Amani ya Palestina, ni Amani ya Tanzania
Wito wa kujitokeza kwa watu wote, Waislamu na Watanzania wote wapenda Haki katika siku ya Kimataifa ya Quds, ili kuungana na Wapalestina katika kutetea Haki zao za Kibinadamu katika Taifa lao la Palestina, na vile yakiwa ni Matembezi ya Masjid Al_Aqsa, ambayo ni Kibla cha Kwanza cha Waislamu.
-
Gwaride la Boti 3,000 za Kijeshi za Iran litafanyika kuwaunga Mkono Wananchi wa Palestina
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran limetangaza Gwaride la Boti za Kijeshi 3,000 na uhamasishaji wa Wananchi kwa ajili ya kuwaunga mkono Wananchi wanaodhulumiwa wa Palestina.
-
Ayatollah Makarem Shirazi:
Maandamano ya Siku ya Quds ni Nguvu ya Moyo kwa Mujahidina na Wanyonge wa Palestina na Lebanon
Ayatollah Makarem Shirazi, Miongoni mwa Marjii Taqlid, amewaalika Waislamu ili kushiriki katika Maandamano ya Siku ya Quds, alifafanua akisema: Ni muhimu kwa viongozi na marais wa nchi za Kiislamu kuazimia na kuhakikisha azma yao ya kuacha kutojali na kupuuzia jinai za Wazayuni.
-
Jumuiya ya walimu wa Seminari ya Qom:
Wananchi wa Iran wanapaswa kutangaza utayarifu wao wa kuwasaidia wapiganaji wa Palestina kwa kushiriki katika maandamano ya Siku ya Quds
Katika kizingiti cha Siku ya Quds Duniani, Jumuiya ya Walimu wa Seminari ya Qom imetoa taarifa ikizitaka sehemu zote za Taifa pendwa la Iran kushiriki kikamilifu katika Matembezi ya Amani ya Siku hii ya Quds na kutangaza kwa mara nyingine uungaji mkono wao kwa Muqawamah (Upinzani) wa Kiislamu wa Palestina.