Wizara
-
Baqaei: Lamerd Ni Alama ya Mapambano na Mateso ya Wairani Dhidi ya Maadui Wakubwa
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Ismail Baqaei, amesema mji wa Lamerd ni ishara ya mapambano, mateso na dhamira ya wananchi wa Iran ya kukabiliana na maadui wakubwa, akisisitiza kuwa ziara yake mjini humo inalenga kuwashukuru wananchi na kukutana na familia za mashahidi.
-
Iran: Baghai Amshutumu Grossi kwa Kudhoofisha Uaminifu wa IAEA
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Ismail Baghai, amemshutumu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA), Rafael Grossi, kwa kutumia ripoti za kitaalamu za wakala huo katika muktadha wa kisiasa, akidai kuwa hali hiyo inahatarisha uaminifu, uhuru na kutokuegemea upande wowote kwa taasisi hiyo.
-
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran: Tutajibu kwa Kuthabiti Uchokozi Wowote wa Kijeshi
Iran imelaani vikali shambulio la Marekani dhidi ya meli za mafuta za Iran katika Ghuba ya Uajemi na Bahari ya Oman, ikisisitiza kuwa Majeshi yake hayatasita kutumia haki yake ya kujilinda na yatajibu kwa uthabiti dhidi ya uchokozi wowote wa kijeshi.
-
Iran Yaitaka Baraza la Usalama la UN Kuwajibika Dhidi ya Mashambulizi ya Israel Nchini Lebanon
Iran imelaani vikali mashambulizi ya Israel dhidi ya Lebanon na kuitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa pamoja na nchi wanachama kuchukua hatua za haraka kukomesha mashambulizi na uhalifu wa kivita unaofanywa dhidi ya raia wa Lebanon.
-
Mkuu wa Jeshi na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Pakistan Waondoka Tehran
Mkuu wa Jeshi na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Pakistan wameondoka Tehran Jumatatu jioni, baada ya kumaliza ziara yao ya siku moja. Mazungumzo yao yalihusu kuimarisha ushirikiano wa pande mbili na Iran, pamoja na maendeleo ya kikanda na umuhimu wa kushirikiana katika kukuza amani, utulivu na usalama wa eneo.
-
Iran: Vita la hivi karibuni yaweka upya vipaumbele na mwelekeo wa viwanda vya ulinzi
Waziri wa Ulinzi wa Iran amesema vita la hivi karibuni limeibua hitaji la kuainisha upya vipaumbele vya sekta ya ulinzi, huku uzalishaji wa baadhi ya vifaa vya kijeshi ukiongezeka hadi mara kadhaa licha ya vita.
-
Iran: Nguvu yetu ya ulinzi inalenga kuzuia vita, si kuvianzisha
Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Iran, Brigedia Jenerali Majid Ibn al-Reza, amesema nguvu ya ulinzi ya Iran inalenga kuimarisha uwezo wa kuzuia vita na kuhakikisha nchi inalindwa, si kuanzisha vita au uchokozi dhidi ya mataifa mengine.
-
Wizara ya Ulinzi Iran: Tutaendelea kwa nguvu na njia ya Kiongozi Shahidi katika kujenga uwezo wa ulinzi wa taifa
Wizara ya Ulinzi ya Iran imesisitiza kuendelea kuimarisha uwezo wa ulinzi wa nchi, kwa kuendeleza njia iliyowekwa na Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, huku ikisisitiza kujitegemea na kutumia uwezo wa vijana, wanasayansi na wataalamu wa Iran.
-
Abbas Araghchi kuzungumzia utendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran kwa miaka miwili iliyopita
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, anatarajiwa kuzungumza kupitia televisheni ya Iran kuhusu utendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.
-
Wizara ya Usalama ya Iran: Ufaransa Ichukue Wajibu kwa Uingiliaji wa Wanadiplomasia Wake
Wizara ya Usalama ya Iran imeionya serikali ya Ufaransa kuacha kuingilia masuala ya ndani ya Iran, ikisema endapo vitendo hivyo vitajirudia, wahusika watachukuliwa hatua zinazofaa.
-
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran: Jaribio lolote la kuupuuza suala la Palestina linakataliwa
Iran imelaani vikali madai ya Waziri Mkuu wa Israel kuhusu umiliki wa kudumu wa Milima ya Golan na kukataa kuanzishwa kwa taifa huru la Palestina, ikisisitiza kuwa hatua za kikoloni haziwezi kubadilisha ukweli wa kihistoria na kisheria.
-
Iran: Seli mbili za makundi ya kigaidi zakamatwa kusini mashariki mwa nchi
Wizara ya Usalama ya Iran imetangaza kukamatwa kwa watu wanne wanaodaiwa kuwa wanachama wa makundi ya kigaidi na kuuawa kwa wengine wawili wakati wa mapambano na vikosi vya usalama katika mji wa Khash, mkoani Sistan na Baluchestan.
-
Baqaei: Ukimya wa Baraza la Usalama Umeitia Moyo Israel Kuendelea na Uhalifu Wake Lebanon
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Ismail Baqaei, amelaani vikali mashambulizi ya Israel dhidi ya kusini mwa Lebanon, akisema ukimya wa taasisi za kimataifa, hususan Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, umeitia moyo Israel kuendelea na mashambulizi na ukiukaji wa mamlaka ya Lebanon.
-
Wizara ya Ulinzi ya Iran: Iran Itaendelea Kuwa Imara na Yenye Nguvu Katika Uwanja wa Ulinzi
Wizara ya Ulinzi na Msaada kwa Vikosi vya Iran imesisitiza kuwa, katika mazingira ya vita mseto na operesheni za kisaikolojia za maadui, waandishi wa habari wana jukumu muhimu katika kusimulia ukweli kwa uaminifu, kulinda maoni ya umma na kuimarisha uwezo wa kitaifa wa kuzuia vitisho.
-
Iran: Mazungumzo na Oman ni ya Pande Mbili, Hayawahusu Wadau Wengine
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa mazungumzo kati ya Iran na Oman ni ya pande mbili na hayahusiani na upande mwingine wowote, akisisitiza kuwa msimamo wa Iran kuhusu Mlango wa Hormuz na maslahi yake ya kitaifa hautabadilishwa na vitisho au shinikizo.
-
Iran Yakumbuka Miaka Miwili Tangu Kuuawa Shahidi kwa Ismail Haniyeh, Yasisitiza Kuendelea Kuunga Mkono Palestina
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imetoa tamko la kumbukumbu ya miaka miwili tangu kuuawa kwa Ismail Haniyeh, ikisisitiza kuendelea kuunga mkono mapambano ya Wapalestina na kutoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua kuhusu hali ya Gaza na Ukingo wa Magharibi.
-
Yemen: Hakuna Atakayezuia Wananchi Wetu Kupata Haki Zao Halali
Wizara ya Mambo ya Nje ya Yemen imesema kuwa hata kama dunia nzima itaungana kuzuia wananchi wa Yemen kupata haki zao halali, jitihada hizo zitashindwa. Aidha, imeituhumu Saudi Arabia kuendelea na mzingiro dhidi ya Yemen na kuonya kuwa uwepo wa kijeshi katika Bahari Nyekundu unaweza kuhatarisha utulivu wa eneo hilo.
-
Iraq yakemea mashambulizi ya anga ya Marekani na Saudi Arabia
Serikali ya Iraq imelaani mashambulizi ya Marekani na Saudi Arabia, ikisisitiza kuwa yanakiuka mamlaka yake. Baraza la Usalama wa Taifa limeagiza kuandaliwa kwa mpango wa kukabiliana na ukiukaji huo, huku Wizara ya Mambo ya Nje ikitakiwa kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria za kimataifa. Iraq pia imeahidi kurekodi matukio hayo na kulinda haki na mamlaka yake ya kitaifa.
-
Iran Yalaani Mashambulizi Yanayodaiwa Kufanywa na Marekani na Saudi Arabia dhidi ya Iraq na Misafara ya Mazuwwari wa Arbaeen
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani vikali mashambulizi yanayodaiwa kufanywa na Marekani na Saudi Arabia dhidi ya maeneo rasmi nchini Iraq na misafara ya kuhudumia mazuwwari wa Arbaeen ya Imam Hussein (as), ikiyataja kuwa ni ukiukaji wa mamlaka ya Iraq na sheria za kimataifa.
-
Zakharova: Dunia nzima sasa imeelewa maana ya “mazungumzo kwa mtindo wa Magharibi”
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi, Maria Zakharova, amesema kuwa dunia nzima sasa imeelewa maana ya mazungumzo kwa mtindo wa Magharibi, akisema kuwa nchi za Magharibi hutumia tuhuma za kutaka kuonyesha kuwa upande mwingine hautaki mazungumzo kama kisingizio cha kuandaa mazingira ya vita.
-
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Auliza: “Yuko Wapi Grossi?” Baada ya Mashambulizi ya Marekani Dhidi ya Vituo vya Nyuklia vya Iran
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Ismail Baghaei, amekosoa ukimya wa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA), Rafael Grossi, kuhusu mashambulizi na vitisho vya Marekani dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran, akisema mashambulizi hayo ni ukiukaji mkubwa wa sheria za kimataifa na kanuni za IAEA.
-
Ismail Baghaei:
Vitisho na Mashambulizi ya Marekani Dhidi ya Vituo vya Nyuklia vya Amani vya Iran ni Ushahidi wa Uadui wa Kina Dhidi ya Sayansi na Maendeleo ya Iran
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Ismail Baghaei, amesema kuwa mashambulizi na vitisho vinavyorudiwa vya Marekani dhidi ya vituo vya nyuklia vya amani vya Iran vinaonyesha uadui wa kina wa Marekani dhidi ya sayansi, maarifa na maendeleo ya Iran.
-
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran: Tutalinda Ardhi Yetu kwa Kutumia Uwezo Wetu Wote
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesema Jamhuri ya Kiislamu itaendelea kutetea uhuru, mamlaka na umoja wa ardhi yake kwa kutumia uwezo wake wote, huku ikiishutumu Marekani kwa kile ilichodai kuwa ni ukiukaji wa makubaliano, kuendeleza mashambulizi na kuvunja sheria za kimataifa.
-
Pakistan yataka utulivu urejee katika Mlango wa Hormuz, yahimiza mazungumzo badala ya mzozo
Wizara ya Mambo ya Nje ya Pakistan imesisitiza umuhimu wa kurejea kwa hali ya kawaida katika Mlango wa Hormuz, ikitaka pande zote kujizuia, kulinda usalama wa usafiri wa baharini na kutoa kipaumbele kwa mazungumzo na diplomasia ili kudumisha amani na utulivu wa kikanda.
-
Iran: Marekani Imekiuka Mara Kadhaa Hati ya Maelewano; Tehran Yasisitiza Haitaanzisha Ukiukaji wa Makubaliano
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesema Hati ya Maelewano kati ya Tehran na Washington inapitia kipindi cha mgogoro, huku ikiishutumu Marekani kwa kukiuka mara kwa mara masharti ya makubaliano hayo na kuhatarisha usalama wa usafiri wa baharini katika eneo.
-
Iran: Utekelezaji wa Makubaliano na Marekani Unategemea Kutekelezwa kwa Ahadi za Washington | Makubaliano hayo Yamekwisha baina ya Iran na Marekani
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesema kuwa utekelezaji wa makubaliano yoyote na Marekani unategemea Washington kutekeleza kikamilifu ahadi zake, huku ikisisitiza kuwa hakuna shaka kuwa makubaliano ya awali ya hati ya maelewano (Memorandum of Understanding) yamefikia mwisho.
-
Iran Yalaani Vikali Shambulio la Kigaidi Kusini Magharibi mwa Pakistan
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Ismail Baqaei, amelaani vikali shambulio la kigaidi lililotokea katika mji wa Khuzdar kusini magharibi mwa Pakistan, akitoa salamu za pole kwa familia za wahanga na kusisitiza umuhimu wa ushirikiano wa kikanda katika kupambana na ugaidi.
-
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran: Njia ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu itaendelea kwa nguvu
Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesisitiza kuwa kuuawa shahidi kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Imam Sayyid Ali Khamenei (Quds Sirruh), si mwisho wa safari, bali ni mwanzo wa hatua mpya ya kuendeleza hadhi ya Uislamu na Iran, huku njia na misingi yake ikiendelea kwa nguvu na uthabiti.
-
Wizara ya Ulinzi Iran Yatangaza Kusambaza Rasilimali Zake Kusaidia Waombolezaji wa Kiongozi Shahidi
Kwa mujibu wa msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Iran, Brigedia Jenerali Tala'inik, wizara hiyo imehamasisha uwezo wake wote katika miji ya Tehran, Qom na Mashhad ili kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi wanaoshiriki shughuli za mazishi ya kiongozi shahidi, ikiwemo huduma za kitabibu, kitamaduni na msaada wa kiutendaji.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi Akutana na Mwenzake wa Iraq Jijini Baghdad
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Seyyed Abbas Araghchi, amewasili Baghdad kwa ziara rasmi na kukutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq, Fouad Hussein, kwa lengo la kujadili masuala ya pande mbili na maendeleo ya kikanda.