Mohammad Abdulsalam, Msemaji wa Harakati ya Ansarullah ameongeza kuwa, haiwezekani kutoa nara na kauli mbio za ubinadamu na kubainisha wasi wasi kuhusu hali mbaya iliyoko Yemen kutokana na mzingiro na vita na kisha wakati huo huo kuendelea kuwauzia wavamizi silaha.
Abdulsalam amesema Marekani inafahamu vyema kile ambacho kitapelekea amani kurejea Yemen. Ameongeza kuwa Marekani inapaswa kuwalazimu wavamizi wa Yemen wasitishe vita na mzingiro wao dhidi ya nchi hiyo ili jitihada za kidiplomasia za kusaka amani ziweze kuzaa matunda.
Kauli hiyo ya Abdulsalam imekuja baada ya Ofisi ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani kuwasiliana na Martin Griffiths, mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Yemen na kubainisha wasiwasi kuhusu hali ya kibinadamu Yemen.