18 Oktoba 2022 - 16:25
Russia yaionya vikali Israel dhidi ya kuipa silaha Ukraine

Rais wa zamani wa Russia ameuonya vikali utawala wa Kizayuni wa Israel na kuutaka usithubutu kuipa silaha Ukraine.

Dmitry Medvedev ambaye ni Naibu Mkuu wa Baraza la Usalama wa Taifa la Russia ametoa indhari hiyo katika ujumbe alioutuma kwenye mtandao wa kijamii wa Telegram na kusisitiza kuwa, kuipa silaha Ukraine ni hatua hatari ambayo imeharakishwa na ambayo haijazingatia matokeo yake mabaya.

Amebainisha kuwa, utawala haramu wa Israel unajiandaa kuipa Ukraine silaha, na iwapo hilo litatokea, uhusiano baina ya Moscow na Tel Aviv utasambaratika.

Mwanasiasa huyo wa Russia ameeleza bayana kuwa, inashangaza Israel inataka kuwapa silaha watu wanaotumia nembo za Kinazi, na wanaopigania fikra na itikadi za Ujerumani ya Kinazi, licha ya kuwa fikra hizo zimewahi kutumia huko nyuma dhidi ya jamii mbalimbali ikiwemo ya Wayahudi.

342/