Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Ahl-ul-Bayt (a.s.) - Abna, Kufuatia kifo cha mke mtukufu wa Ayatullah al-Udhma Sayyid Ali Sistani, Kiongozi Muadhamu, Hadhrat Ayatullah al-Udhma Khamenei, alitoa rambirambi zake kwa Marja' huyu mkuu kupitia ujumbe.
Ujumbe kamili wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ni kama ifuatavyo:
Bismillahir Rahmanir Rahim (Kwa Jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu)
Hadhrat Ayatullah Sayyid Ali Sistani (Damat Barakatuh - Baraka zake zizidi)
Natoa rambirambi zangu kwa ajili ya kifo cha mke wako mtukufu na ninamuomba Mwenyezi Mungu amrehemu na amsamehe.
Sayyid Ali Khamenei | 7 Mehr 1404
Your Comment