Kwa mujibu wa shirika la habari la ABNA likinukuu Al-Mayadeen, Brigedia Jenerali Abed al-Thaur, mmoja wa maafisa wa harakati ya Ansarullah, amesisitiza: "Sanaa inafuatilia kwa karibu maendeleo ya kusini mwa Yemen na inapinga uchokozi wowote dhidi ya nchi hii."
Aliongeza: "Kinachotokea kusini mwa Yemen ni njama ya Imarati na Saudia kwa kufuata maagizo ya Marekani na utawala wa Kizayuni. Saudi Arabia inataka kuchukua udhibiti wa mkoa wa Hadramout kwa ajili ya kusafirisha mafuta kupitia Bahari ya Arabia, wakati Imarati inatafuta kudhibiti bandari za kusini mwa Yemen."
Inafaa kumbuka kuwa kwa wiki kadhaa sasa, mapigano kati ya mamluki wa Imarati na Saudi Arabia yamepamba moto katika maeneo ya mashariki na kusini mwa Yemen, jambo ambalo limeifanya Marekani kuelezea wasiwasi wake.
Your Comment