Kwa mujibu wa shirika la habari la ABNA kwa kunukuu Ma'a, mke wa Itamar Ben-Gvir, waziri wa usalama wa ndani wa utawala wa Kizayuni, alisherehekea siku yake ya kuzaliwa ya miaka 50 kwa kutoa keki yenye utata.
Kwa mujibu wa ripoti hii, keki ya siku ya kuzaliwa ya Ben-Gvir ilipambwa kwa alama ya mnyongoo, inayoashiria sheria yenye utata ya kunyonga wafungwa wa Kipalestina. Juu ya keki hiyo iliandikwa: "Wakati mwingine ndoto hutimia!"
Sherehe hiyo ilihudhuriwa na maafisa wakuu wa polisi wa utawala wa Kizayuni na wanausalama wa utawala huu. Wapinzani katika utawala wa Kizayuni walisisitiza kuwa sherehe hii ilibeba zaidi ujumbe wa kisiasa na wa uchochezi.
Muda mfupi uliopita, Knesset (bunge) la utawala wa Kizayuni kwa hatua ya uadui na isiyo ya utu, liliidhinisha rasimu ya sheria ya kunyongwa kwa wafungwa wa Kipalestina kwa kura nyingi.
Rasimu hii ilipitishwa wakati asasi za haki za binadamu zilikuwa tayari zimetahadharisha kuhusu matokeo hatari na ukiukaji mkubwa wa sheria za kimataifa na utawala wa Kizayuni dhidi ya wafungwa.
Your Comment