Kwa mujibu wa ABNA, gazeti la Marekani la Wall Street Journal kwa kunukuu vyanzo vyenye ufahamu liliripoti kwamba serikali ya Trump licha ya kufanikiwa kufanya baadhi ya mafanikio ya kimbinu katika vita, haikutimiza lengo lolote la kimkakati katika vita dhidi ya Iran.
Vyanzo hivi vilisema kwamba bado kuna mapengo makubwa kati ya misimamo ya Washington na Tehran kuhusu usimamizi wa baadaye wa Mlango wa Hormuz.
Viliviongeza kuwa kuna mapengo makubwa pia kuhusu aina ya vikwazo ambavyo Tehran itakubali katika mpango wake wa nyuklia.
Gazeti la Marekani lilikiri kwamba Donald Trump katika uchochezi wake wa vita dhidi ya Iran hakufanikiwa kufanya lengo lolote kati ya malengo yake ya kimkakati.
Your Comment