19 Mei 2026 - 10:58
Source: ABNA
Erdoğan: Vita dhidi ya Iran vimeuweka mkoa katika ukingo wa machafuko

Rais wa Uturuki kwa maneno makali alielezea athari mbaya za mashambulio ya pamoja ya Marekani na Israel dhidi ya Iran pamoja na uvamizi wa hivi karibuni wa Kizayuni huko Gaza.

Kwa mujibu wa shirika la habari la ABNA kwa kunukuu kituo cha Russia Today, Recep Tayyip Erdoğan, Rais wa Uturuki, baada ya kumalizika kwa kikao cha baraza la mawaziri katika Ikulu ya Rais huko Ankara, alisisitiza: "Vita vya Februari 28 (9 Esfand) vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vimeuweka mkoa katika ukingo na kizingiti cha machafuko na mtikisiko kamili."
Alisema: "Kwa sasa, kiwango kamili cha uharibifu kutokana na mashambulio ya Marekani na Israel dhidi ya Iran bado hakiwezi kukadiriwa."
Erdoğan aliongeza: "Mitikio inayotokana na mgogoro huu inaendelea na inajidhihirisha katika kupanda kwa kasi kwa bei, hasa katika sekta ya nishati."
Rais wa Uturuki alibainisha: "Moto wa vita hivi ingawa haukutugusa moja kwa moja, lakini moshi wake unatudhuru macho yetu."
Alisisitiza: "Kwa kuchukua msimamo wa utulivu, upole, wa hadhi na wa busara, tumeweza kukabiliana na njama zilizokuwa zikijaribu kuiturumbukiza Uturuki katika vita hivi."
Kuhusu suala la Palestina, Erdoğan alisisitiza kwamba Uturuki itasalia kando ya Palestina dhidi ya uvamizi huu wa Israel mpaka mwisho.
Rais wa Uturuki hatimaye alikumbusha kwamba wakati dunia ya leo imekuwa kimataifa na migogoro na mizozo ikizigubika nchi zote na pande zote bila ubaguzi, katika hali hii hakuna nchi yoyote inayoweza kufumbia macho matukio yanayoendelea duniani.

Your Comment

You are replying to: .
captcha