5 Juni 2026 - 13:22
Source: ABNA
Sardar Hassanzade: Wamarekani walishindwa siku ya kumi ya Vita vya Ramadhani

Kamanda wa Kikosi cha Muhammad Rasulullah (s.a.w.) Tehran alisema: "Trump na Wamarekani walishindwa siku ya kumi ya vita, na kwamba mnaona mabadiliko kadhaa katika misimamo, hii ni kwa sababu adui ameshindwa kweli."

Sardar Hassan Hassanzade, Kamanda wa Kikosi cha Muhammad Rasulullah (s.a.w.) Tehran, katika mazungumzo, kuhusu uwezo wa kivita na uwezo wa kushambulia na kujitetea wa Kikosi kwa ajili ya kukabiliana na uovu wowote wa adui wa Marekani na Kizayuni, alisema: "Ingawa si kawaida kutangaza uwezo wetu wote, lakini adui anajua kwamba katika kila mapigano aliyoingia nasi, amekutana na uwezo, nguvu na kadi za ushindi kutoka kwetu ambazo hakuwahi kukutana nazo hapo awali."
Aliongeza: "Watu wetu wajue kwamba katika siku zijazo, kama adui atataka kufanya kosa tena, hakika atakabiliana na matukio ambayo yatamshangaza tena na kumdunisha. Kwa hiyo, tunawapa watu wetu ahadi kwamba maandalizi [ya vikosi vyetu vya silaha] ni makubwa zaidi kuliko mwanzoni mwa Vita vya Ramadhani na Vita vya tatu vya kulazimishwa."
Kamanda wa Kikosi cha Muhammad Rasulullah (s.a.w.) Tehran aliendelea: "Kwa kawaida, katika vita hivi vyote mlivyoviona, tumewashangaza maadui mbele ya watu wetu, azma ya watu wetu na wapiganaji wetu."
"Dharma zote na makadirio ya adui katika vita dhidi ya Iran hayajatimia"
Alisema: "Dharma zote na makadirio aliyokuwa nayo hadi leo, sio tu kwamba hayajatimia na kufikia malengo hayo, bali zaidi ya hayo, tumepata faida za ziada katika uwanja ule ule ambao adui alikuwa amelenga."
"Adui amedhalilishwa na hana jibu kwa wasomi wake na wataalamu wake"
Hassanzade, akizungumzia ukweli kwamba dunia na eneo limekubali kushindwa kwa Amerika na ushindi wa Iran, alisema: "Kwa maoni yangu, Trump na Wamarekani walishindwa siku ya kumi ya vita, na kwamba mabadiliko kadhaa katika tabia na misimamo mnayoyaona sasa, ni kwa sababu maadui wetu wameshindwa kweli na kudhalilishwa mbele ya azma ya watu wetu na nguvu ya vikosi vyetu vya silaha, na hawana jibu mbele ya watu wao, wasomi wao, wataalamu wao na watu wa dunia."
Alisema: "Leo, kwa neema ya Mola, dunia nzima inajua kwamba upande ulioshinda uwanjani ni watu wa Iran, mbele ya upinzani na Iran ya Kiislamu, na wote wanajua kwamba Wamarekani na utawala wa Kizayuni wameshindwa kwa asilimia 100 katika malengo yao, na kwa kawaida lazima wakubali kwamba wapige magoti mbele ya watu wetu na wasalimu amri kwa azma hii ya chuma ambayo imekuwa ikijitokeza kwenye viwanja kwa usiku zaidi ya tisini."

Your Comment

You are replying to: .
captcha