Kwa mujibu wa shirika la habari la Abna, Joe Kent, Mkurugenzi wa zamani wa Kituo cha Kitaifa cha Marekani cha Kupambana na Ugaidi, akizikosha sera za Washington dhidi ya Iran, alichapisha ujumbe kwenye mtandao wa kijamii X na kusisitiza: Kama lengo letu lingekuwa ni kutokua, tungeliharibu kwa upumbavu juhudi zetu za kufikia lengo hilo.
Akirejelea uvamizi wa Marekani na mauaji ya kiongozi shahidi, alisisitiza: Kwa kumuua (na kumshahidi) Ayatollah na kushambulia Iran, tumeonyesha kwamba mkakati wao - kutotengeneza silaha za nyuklia na kudumisha uwezo wa kurutubisha urani - hautoshi kuzuia uvamizi wa Marekani.
Kent aliongezea: Sasa, kama utabadilisha jina la Iran na kuweka Korea Kaskazini, tumeithibitishia dunia kwamba kitu pekee kinachozuia shambulio la Marekani ni silaha za nyuklia.
Maoni yako