18 Desemba 2014 - 17:56
Umoja wa Ulaya kuiwekea Urusi vikwazo vipya

Umoja wa Ulaya umekubaliana kuweka vikwazo vipya dhidi ya jimbo lililochukuliwa na Urusi la Crimea kuonesha msimamo wake dhidi ya Urusi,

Umoja  wa  Ulaya  umekubaliana  kuweka  vikwazo  vipya  dhidi  ya jimbo  lililochukuliwa  na  Urusi  la  Crimea kuonesha  msimamo wake  dhidi  ya  Urusi, wakati viongozi  wa  Umoja  wa  Ulaya wakijitayarisha  kujadili  mzozo  unaoongezeka  wa  kifedha  nchini Urusi huku  kukiwa  na  hofu  za  athari  katika  uchumi  wa  mataifa hayo.

Viongozi  hao  ambao  wanakutana  mjini  Brussels  pia  wanaunga mkono mpango  wa  uwekezaji  wa  euro  bilioni  315 wenye  lengo la  kuchochea  uchumi  wa  mataifa  ya  Ulaya  unaodorora, licha  ya kuwa  ahadi  za  fedha  taslimu hazitarajiwi  kutolewa.

Mkutano  huo  wa  kwanza  kuongozwa  na  rais  mpya  wa  baraza la  Ulaya  Donald Tusk , kiongozi  wa  zamani  wa  Poland , unakuja huku  kukiwa  ya  hali  ya  kuporomoka  kwa  sarafu  ya  Urusi  ya rouble kutokana  na  vikwazo  vya  mataifa  ya  magharibi  na kupungua  kwa  bei  ya  mafuta.

Kansela  wa  Ujerumani  Angela  Merkel amesema  kabla ya  kwenda mjini  Brussels  kwamba  vikwazo  vya  mataifa  ya  magharibi  dhidi ya  Urusi  havikwepeki hadi  pale rais Vladimir Putin atakaporuhusu Ukraine  huru  na  iliyoungana.

Rais wa Urusi amelihutubia taifa lake na kuwaambia kuwa wasiwe na wasi kwani haya ni matatizo ya muda mfupi tu na kwamba uchumi wa Urusi utakuwa wa hali ya juu muda si mrefu,pia ameituhumu Marekani na Saudia Arabia kwa kushusha bei ya mafuta makusudi kwa lengo la kudhoofisha uchumi wa Iran na Urusi.

 

Tags