-
Sala ya Ijumaa - Jamiat Al-Mustafa (s) - Dar-es-salaam - Tanzania | Fadhila za Mwezi wa Dhilhijja na Aamali Zake Muhimu + Picha
Sayyid Mansour Al-Musawiy alisisitiza kuhusu utukufu wa Mwezi wa Dhilhijja, hasa siku zake kumi za mwanzo ambazo zimepewa heshima kubwa katika mafundisho ya Kiislamu. Alieleza kuwa hizi ni siku adhimu ambazo Mwenyezi Mungu ameapa kwazo katika Qur'an Tukufu (Surat al-Fajr: 2 – "Na kwa masiku kumi!"), na kwamba ndani yake kuna fursa kubwa kwa Muumini kujikurubisha kwa Mola wake kwa kukithirisha Ibada kama vile: Kuswali sana, kusoma Qur'an, kufanya dhikri (kumkumbuka Mwenyezi Mungu) na kuomba dua mbalimbali.
-
Macron: Kuitambua rasmi Palestina kama nchi huru ni jambo la dharura
Kufuatia kushadidi mashambulio ya Israel dhidi ya Gaza, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, amesisitiza haja ya kutambuliwa rasi Palestina kama taifa.
-
Je, kubadilika mkakati wa kijeshi wa Marekani barani Afrika, ni kurudi nyuma au kubadilishwa mbinu?
Jeshi la Marekani linaendelea kubadilisha na kulegeza misimamo yake ya awali kuhusu "utawala bora" barani Afrika na kukabiliana na vyanzo vya uasi na machafuko, na sasa linasisitiza kwamba serikali dhaifu za Kiafrika zinazoshirikiana na Marekani zinapasa kujitegemea zenyewe kijeshi na kiusalama.
-
Saudia, Qatar, UAE zamuonya Trump asithubutu kuanzisha vita na Iran
Tovuti ya habari ya Axios ya Marekani imeripoti kuwa, viongozi wa Saudi Arabia, Qatar, na Imarati (UAE) walipinga vikali shambulizi lolote dhidi ya Iran wakati walipoonana na Trump na kuonya juu ya madhara yake yasiyotabirika kwa washirika wa Marekani kwenye eneo hilo.
-
Ni jinai gani nyingine imebakia haijafanywa na Israel
Maafa ya kibinadamu huko Ghaza Palestina yamefika kileleni kiasi kwamba katika uhalifu wa karibuni zaidi wa Israel, jeshi katili la utawala wa Kizeyuni limeshambulia vituo vya usambazaji chakula ambavyo Israel yenyewe ilikubali viwepo na mpaka iliainisha viwekwe maeneo gani.
-
Je, utawala wa Trump unataka kubadilisha kisiasa mazingira ya vyuo vikuu vya Marekani?
Kutokana na hali ya mvutano inayoendelea kati ya utawala wa Rais Donald Trump wa Marekani na Chuo Kikuu cha Harvard, serikali imetaka kufutwa kwa kandarasi zote za kifedha na chuo hicho.
-
Vikosi vya Yemen vyashambulia uwanja wa ndege Israel kwa kombora la kasi ya juu
Vikosi vya kijeshi vya Yemen vimeendesha operesheni nyingine dhidi ya utawala dhalimu wa Israel, kwa kulenga Uwanja wa Ndege wa Ben Gurion kwa kombora la kasi ya juu (hypersonic) ikiwa ni jibu kwa mashambulizi ambayo Israel inaendeleza dhidi ya Wapalestina huko Gaza.
-
Mkuu wa UNRWA: Waarabu wawape Wapalestina sehemu ndogo ya Matrilioni waliyompa Trump
Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa Linalowahudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) amezitaka nchi za Kiarabu katika Ghuba ya Uajemi kutenga sehemu ndogo tu ya fedha zilizotajwa katika ‘makubaliano makubwa’ kati yao na Rais wa Marekani, Donald Trump, ili kusaidia wakimbizi wa Kipalestina wanaopambana kuendelea kuishi katika ardhi zao ambazo Israel imezikalia kwa mabavu na pia wale wanaoishi katika nchi jirani.
-
Ireland yasisitiza Israel inatekeleza mauaji ya kimbari Gaza
Katika mjadala mkali uliotikisa bunge la Ireland, naibu waziri mkuu Simon Harris, ametetea msimamo wa serikali kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel unatekeleza mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina huko Gaza.
-
Iran yakanusha taarifa za kukaribia makubaliano na Marekani
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesisitiza dhamira ya Tehran ya kuendelea kushiriki katika mchakato wa kidiplomasia, huku akilaani kile alichokieleza kuwa ni upotoshaji wa vyombo vya habari unaolenga kuvuruga mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja yanayoendelea kati ya Iran na Marekani kuhusu mpango wa nyuklia wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Rais Pezeshkian: Silaha za nyuklia hazina nafasi katika doktrini ya Jamhuri ya Kiislamu
Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesisitiza kuwa, Iran kamwe haitaacha haki yake ya kisheria ya kurutubisha madini ya urani.
-
Umoja wa Mataifa: Gaza ndio eneo lenye njaa zaidi duniani
Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) imelitaja Ukanda wa Gaza kuwa eneo lenye njaa kubwa zaidi duniani na kutangaza kuwa shirika hilo liko tayari mara moja na kwa kiwango kikubwa kupeleka misaada ya kibinadamu katika eneo hilo.
-
Ayatullah Khatami: Iran katu haitalegeza msimamo kwa haki yake ya matumizi ya nishati ya nyuklia kwa malengo ya amani
Imamu wa muda wa Swala ya Ijumaa mjini Tehran amesema kuwa, Iran katu haitalegeza msimamo kwa haki yake ya matumizi ya nishati ya nyuklia kwa malengo ya amani.
-
Sala ni Nguzo ya Dini - Na Kuswali Sala ya Ijumaa ni Kuimarisha na Kuhuisha Ahadi na Mwenyezi Mungu + Picha
Katika Khutba za Ijumaa, Imam alikumbusha kuwa: Kuswali Sala Al-Jum’a ni moja ya dalili za mshikamano wa Kiislamu na ni fursa ya kila wiki ya kuhuisha Ahadi ya kumtii Mwenyezi Mungu(SWT), pamoja na kuongeza uelewa wa Dini na Jamii katika mioyo ya Waumini.
-
Hujjatul-Islam, Sheikh Ghawth: "Uislamu na Heshima ya Mwanamke | Wanawake ni Nguzo Muhimu Katika Tablighi ya Kiislamu" + Picha
Baada ya kuja kwa Mtume wa Uislamu (S.A.W.W), Hadhi ya Mwanamke ilipandishwa kwa kiwango kikubwa. Mfano wa wazi ni Malezi ya Bibi Fatima Zahra (S.a) aliyolelewa na Mtume mwenyewe(S.A.W.W), na kuwa kigezo bora kwa Waislamu wote.
-
Dar es Salaam, Tanzania - Mei 2025:
BAKWATA Yatangaza Rasmi Tarehe ya Sikukuu ya Eid El-Adh’ha: Jumamosi, Juni 7, 2025
Taarifa hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa BAKWATA, Alhaj Nuhu Jabiri Mruma, ambapo imeelezwa kuwa sherehe za kitaifa za Eid El-Adh’ha mwaka huu zitafanyika jijini Dar es Salaam, katika Msikiti wa Mfalme Mohamed VI uliopo Makao Makuu ya BAKWATA – Kinondoni.
-
Mada ya Ijumaa Masjidul Ghadir Kigogo Post: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi (ya Watoto na Jamii)"
Tarehe: Ijumaa, 30 Mei 2025. Mahali: Masjidul Ghadir, Kigogo Post – Dar-es-Salaam, Tanzania. Khatibu wa Swala ya Ijumaa: Maulana Sheikh Hemed Jalala. Mada ya Khutba ya Ijumaa: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi". Khutba hii iliangazia Nafasi ya Hijjah kama Shule ya Malezi ya kina, ikihimiza wazazi na jamii kwa ujumla kutumia mafundisho ya Hijjah kuwalea watoto katika misingi ya Utii, Ucha Mungu, Uvumilivu, Unyenyekevu na Umoja. Pia, iliweka msisitizo wa umuhimu wa Mwezi wa Dhilhijja katika historia ya Uislamu na fadhila za ibada ndani yake.