Sheikh Ravil Ainuddin aliandika katika ujumbe huu: Kwa niaba ya Idara ya Masuala ya Dini ya Waislamu wa Shirikisho la Urusi na masheikh wa kiroho wa nchi yetu, natoa pole kwa wananchi wa nchi hii kwa kuuawa Shahid Sayyid Hassan Nasrullah, Katibu Mkuu wa Hezbollah, huko Beirut.
Katika ujumbe huu, Mufti Mkuu wa Russia amemuomba Mwenyezi Mungu (s.w.t) amjaalie Shahidi Nasrullah kuwa katika daraja za juu za kimungu.
Sheikh Ain al-Din aliendelea na ujumbe huu na kuandika:
Tunaomboleza mamia ya wahanga wa Lebanon kutokana na mashambulizi ya ndege za kivita za Israel katika siku za hivi karibuni.
Aliongeza kusema:
Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema azirehemu roho za ndugu zetu ambao ni wahanga wa uvamizi wa Israel na awape malipo mema ya milele.