Ansarullah
-
Onyo kutoka kwa Kiongozi wa Ansarullah:
Kiongozi wa Ansarullah wa Yemen, akifichua ukubwa wa mauaji ya kimbari na uharibifu wa miundombinu huko Gaza, ametaja pia mipango ya upanuzi ya utawala wa Kizayuni katika eneo la kikanda, ikiwemo Lebanon, Syria na uvamizi wa hivi karibuni dhidi ya Qatar. Ameitaja Marekani kuwa mshirika katika uhalifu huu na kusisitiza kuendelea kwa mapambano na mshikamano wa Kiislamu katika kukabiliana na uchokozi huu.
-
Ujumbe wa Rambirambi kutoka kwa Ayatullah Akhtari kwa Sayyid Abdul Malik al-Houthi: Shambulio la Israel Nchini Yemen ni Jinai Mpya ya Kivita
"Ninatoa rambirambi zangu za dhati kwa watu wa Yemen mashujaa na kwa uongozi wake jasiri – ukiwemo wewe ndugu yetu mpendwa, Sayyid Abdul Malik – kwa msiba huu mkubwa wa kifo cha Shahidi Ahmad Ghalib al-Rahwi na wenzake waliouawa kwa udhalimu na usaliti wa utawala haramu wa Kizayuni.”
-
Maafisa wa Kiyemeni katika mazungumzo na Abna:
"Madai ya Israel ni udanganyifu na kupindisha mambo ili kufidia udhaifu katika uwanja wa mapambano / Msaada kwa Gaza hautasitishwa"
"Abdulaziz al-Bakr", Katibu Mkuu wa chama cha "Ujamaa wa Kitaaluma wa Kiyemen" na "Hizam al-Asad", mjumbe wa ofisi ya kisiasa ya harakati ya Ansarullah ya Yemen, katika mazungumzo na shirika la habari la Abna wamesisitiza kuwa: Kila shambulio linalolenga raia wasio na hatia huko Sana'a linageuka kuwa mafuta ya ziada kwa ajili ya harakati ya mapambano ya wananchi wa Yemen.
-
Sayyid Abdul-Malik Badruddin al-Houthi:
Sera ya makusudi ya kuwalisha watu njaa inayotekelezwa na Wazayuni ni Kushindwa kwa Maadili kwa jamii ya Kimataifa.Magharibi ni Msaidizi Mkuu wa Uovu
"Adui, kwa kushirikiana na Wamarekani, kila siku anaeneza mitego ya mauti kwa lengo la kuwaangamiza Wapalestina, na anaendelea kutekeleza uhalifu wa karne na fedheha ya enzi hii, kwa sababu amepewa uhakikisho kutoka kwa baadhi ya tawala za Kiarabu - bali anapewa motisha, msaada na uungwaji mkono nao."
-
Shambulio Kubwa la Anga la Israel Dhidi ya Mji Mkuu wa Yemen – Ansarullah Yasema Itaendelea Kuunga Mkono Gaza
Vyombo vya habari vya Israel vimeripoti kuwa vyombo vya ujasusi vya Tel Aviv vinaandaa orodha kubwa ya malengo mapya nchini Yemen kwa mashambulizi yajayo.
-
Abdulmalik al-Houthi Awashutumu Waislamu Bilioni Mbili kwa “Kukaa Kimya” Kuhusu Matukio ya Gaza
Katika hotuba yake, al-Houthi alieleza kwa masikitiko na ghadhabu hali ya “kutochukua hatua” kwa Waislamu zaidi ya bilioni mbili duniani, akisema kuwa ukimya huo ni “aibu na fedheha” inayoweza kuleta madhara si tu kwa Palestina, bali pia kwa ulimwengu mzima wa Kiislamu.
-
Sayyid Abdul Malik al-Houthi, amesema: "Fungueni njia kuelekea Palestina. Yemen iko tayari Kijeshi kwenda kuisaidia Palestina"
"Huu ni wakati wa Jihad, na taifa letu la Yemen liko tayari kwa mamia ya maelfu ya wapiganaji kuisaidia Palestina.
-
Mafanikio mawili ya Yemen ndani ya siku moja; Mashambulizi ya Kimaonyesho dhidi ya Hodeidah yazimwa na kushindwa/Meli "Magic Seas" Yazamishwa Baharini
Yemen, imefanikiwa kuitwanga meli iliyokuwa ikielekea maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu na utawala haram wa Kizayuni, na kuizamisha baharini.
-
Katika makala maalum ilijadiliwa:
Ustadi wa Kijeshi wa Waislamu wa Yemen ulivyolazimisha Marekani kufikia makubaliano? Hadithi ya Meli za Vita za Marekani - Ghuba ya Uajemi - yatoweka
Leo, Yemen imethibitisha kwa imani kwamba Marekani imepoteza heshima na hadhi yake, na imeweka mwisho kwa hadithi ya meli za kubeba ndege za kivita za Marekani ambazo zilikuwa zikiziogopesha dunia na nchi washindani wao.
-
Kwa mujibu wa Qur'an Tukufu: Kundi la Mwenyezi Mungu, linalomtii Mwenyezi Mungu, Mtume Wake, na waliokuwa Waumini wa kweli, Hao ndio washindi wa kweli
"Hezbollah" humaanisha: Kundi lililojifunga na miongozo ya Mwenyezi Mungu, linalosimama na kutetea haki, hata likiwa ni dogo au linakabiliwa na maadui wakubwa. Aya hii imekuwa nembo ya Harakati za Muqawama (Upinzani wa Kiislamu) kama vile Hezbollah ya Lebanon, Ansarullah ya Yemen, na wengineo wanaopambana dhidi ya dhulma ya mabeberu ya Kimataifa.
-
Sayyid Abdul Malik al-Houthi: Meli za Marekani ni marufuku pia kupita Bahari Nyekundu
Katibu Mkuu wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema: Tutajibu ongezeko la mvutano kwa ongezeko la mvutano. Kuanzia sasa, sambamba na kupiga marufuku kupita kwa meli za Israeli katika Bahari Nyekundu, kupita kwa meli za Marekani pia ni marufuku.
-
Ansarullah: Tutabaki na Gaza kwa gharama yoyote ile
Mjumbe Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Ansarullah amesisitiza kuwa, Yemen haitaacha kuiunga mkono Palestina kwa gharama yoyote ile na akasema: Kila mtu anajua kuwa Yemen ni Mwaminifu katika kujibu hujuma ya adui, na Marekani inapaswa kusubiri jibu la Yemen.