Sayyid Ali Khamenei
-
Maulana Sheikh Hemed Jalala Atoa Mafunzo Matano Muhimu Kutokana na Mazishi ya Sayyid Ali Khamenei
Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Shia Tanzania (TIC), Maulana Sheikh Hemed Jalala Mwakindenge, amesisitiza umuhimu wa umoja wa Mashia, Waislamu na watu wa dini mbalimbali, pamoja na uzalendo na kuheshimu viongozi wanaolitumikia taifa na jamii kwa uadilifu.
-
Bayani / Taarifa ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (as):
Kuuawa Shahidi kwa Kiongozi Mkuu wa Waislamu kulikuwa Mwanzo wa Biitha Mpya ya watu wa Iran na Umma wa Kiislamu
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (as), akitoa taarifa kwa mnasaba wa kuuawa na kuzikwa kwa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, amelitaja tukio hilo kuwa ni msiba usioweza kurekebishwa kwa Uislamu, Taifa la Iran na Umma wa Kiislamu, na ameielezea safari ya kihistoria ya kuaga ya makumi ya mamilioni ya watu katika miji mitano ya nchi mbili kuwa ni ishara ya “Biitha mpya ya umma” na azma ya Waislamu ya kuendeleza mapambano dhidi ya ubeberu na utawala wa Kizayuni chini ya uongozi wa mrithi mwema wa Kiongozi huyo.
-
Meya wa Tehran: Trump hatakuwa salama popote duniani baada ya mauaji ya Kiongozi wa Iran
Meya wa Tehran, Alireza Zakani, amesema kuwa wale wanaohusika na kuuawa kwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, watakabiliwa na hatua za kulipiza kisasi, akisema kuwa Rais wa Marekani Donald Trump "hatakuwa salama popote duniani."
-
Khatibu wa Ijumaa Tehran: Imam Shahidi alivunja nguvu za ubeberu wa kimataifa
Khatibu wa Swala ya Ijumaa mjini Tehran amesema kuwa Imam Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei (r.a.) alichagua njia ya jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu na, kupitia mapambano yake kabla na baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu, aliweza kuvunja nguvu za ubeberu wa kimataifa.
-
Kumbukumbu ya Shahidi Sayyid Ali Khamenei | Ikhlasi kwa Mwenyezi Mungu Ndiyo Siri ya Athari ya Kudumu
Ujumbe huu unaotolewa katika mnasaba wa kumbukumbu ya Shahidi Ali Khamenei unasema hivi kuwa "Ikhlasi kwa Mwenyezi Mungu ndiyo msingi wa kudumu kwa matendo mema", huku ukisisitiza kwamba athari ya kweli huzaliwa na nia safi ya kumtumikia Allah (swt).
-
Ayatullah Mujtaba al-Husseini Khamenei: Shahidi Aliishi na Kupigania Njia ya Imam Hussein (AS)
Ayatullah Sayyid Mujtaba al-Husseini Khamenei amesema kuwa kiongozi shahidi aliishi, akafikiri, akapambana na hatimaye akapata shahada kwa kufuata kwa dhati njia na mafundisho ya Imam Hussein (AS).
-
Balozi Mdogo wa Iraq nchini Iran: Kuuawa Shahidi kwa Ayatullah Khamenei ni Msiba Unaouhuzunisha Ulimwengu wa Kiislamu
Balozi Mdogo wa Iraq nchini Iran, Athir Al-Abadi, amesema kuuawa shahidi kwa Ayatullah al-Udhma Sayyid Ali Khamenei ni pigo kubwa kwa Umma wa Kiislamu, akimtaja kuwa kiongozi aliyelitumikia dini ya Uislamu kwa kujitolea na kutetea maadili na misingi ya haki.
-
Wizara ya Usalama ya Iran Yapongeza Mahudhurio Makubwa ya Umma wa Kiislamu Katika Mazishi ya Kiongozi Shahidi
Wizara ya Usalama ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa taarifa ya kupongeza ushiriki mkubwa wa wananchi, Marjaa wa dini, serikali na wajumbe kutoka nchi mbalimbali za Kiislamu katika mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, ikieleza kuwa tukio hilo limeonyesha umoja, uaminifu na mshikamano wa Umma wa Kiislamu.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mujtaba al-Husseini Khamenei, Atoa Tamko Maalumu Kufuatia Mazishi ya Imam Shahidi Sayyid Ali Khame
Katika tamko lake kufuatia mazishi makubwa ya Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mujtaba al-Husseini Khamenei, amesisitiza kuendelezwa kwa njia ya Imam Husayn (a.s.), kulinda urithi wa Mapinduzi ya Kiislamu, na kuendelea kudai haki kwa damu za mashahidi.
-
Msemaji wa Serikali ya Iran: Umoja Ndio Urithi Mkuu Aliouacha Imam Shahidi kwa Iran na Ulimwengu wa Kiislamu
Msemaji wa Serikali ya Iran, Fatemeh Mohajerani, amesema kuwa umoja ndio urithi muhimu zaidi aliouacha Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei kwa Iran na ulimwengu wa Kiislamu, akisisitiza kuwa tofauti za maoni hazipaswi kuudhoofisha urithi huo wa thamani.
-
Chuo cha Al-Mustafa (s) Tanzania Kuaandaa Kongamano la Kielimu Kumuenzi Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei(ra)
Kitengo cha Utafiti wa Kisayansi cha Chuo Kikuu cha Al-Mustafa (s) Tawi la Dar es Salaam - Tanzania kitaandaa Kongamano la Kielimu lenye anuani "Imam Khamenei: Kutoka Jihadi hadi Ushahidi," likiwa na lengo la kuchambua kwa ufupi Maisha ya Kiongozi huyo wa Mapinduzi ya Kiislamu, na hatimaye kukuachia msikilizaji na mfuatiliaji Nafasi ya kupata mazingitio na masomo mbalimbali ya kimaisha kutoka katika kumbukumbu ya Maisha yake Matukufu, katika muktadha ule ule wa Maelekezo ya Qur'an Tukufu aliposema Mwenyezi Mungu: Hakika kuna mazingatio ndani ya visa vyao (Historia Yao) kwa watu wenye Akili"
-
Mamia ya Watunisia Waandaa Mazishi ya Mfano kwa Heshima ya Kiongozi Shahidi Imam Sayyid Ali Husseini Khamenei
Mamia ya wananchi wa Tunisia walifanya mazishi ya mfano kwa heshima ya Kiongozi Shahidi Imam Sayyid Ali Husseini Khamenei, wakithibitisha mshikamano wao na mhimili wa muqawama na kupinga kuhalalishwa kwa uhusiano na utawala wa Kizayuni.
-
Kamanda Mkuu wa IRGC: Mazishi ya Kihistoria Iran na Iraq Yamehuisha Ahadi kwa Njia ya Kiongozi Shahidi
Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema kuwa ushiriki wa mamilioni ya watu katika mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran na Iraq ulikuwa ni ishara ya kuhuisha ahadi kwa misingi na njia yake, pamoja na kudhihirisha mshikamano wa Umma wa Kiislamu.
-
Rais Pezeshkian Aishukuru Iraq kwa Kuandaa Mazishi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Sayyid Ali Khamenei (ra)
Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, ameishukuru serikali na wananchi wa Iraq kwa mapokezi na ushirikiano walioutoa wakati wa shughuli za kuaga na kusafirisha mwili wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, akisema taifa la Iran halitasahau kamwe mshikamano huo.
-
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya: Iran Haitaruhusu Uingiliaji wa Usimamizi wa Mlango wa Bahari wa Hormuz
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (s) yametangaza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitaruhusu kwa hali yoyote uingiliaji wa mamlaka yoyote katika usimamizi wa Mlango wa Bahari wa Hormuz, huku yakiahidi kutoa jibu kali dhidi ya kile ilichokitaja kuwa uchokozi wa Marekani.
-
Mwandishi wa Al-Wifaq: Sayyid Ali Khamenei ameanza ukurasa mpya katika nyoyo za wafuasi wake
Mwandishi wa jarida la Al-Wifaq amesema kuwa kwa wafuasi wake, Shahidi Sayyid Ali Khamenei si kiongozi aliyemaliza maisha yake, bali ni fikra na mradi unaoendelea kuishi katika nyoyo na dhamira za Umma.
-
Msanii wa Iran: Shahidi Sayyid Ali Khamenei alitupanda ndani yetu mapenzi ya sanaa na ukweli
Msanii wa Iran Hussein Esmati amesema kuwa kufariki shahidi kwa Sayyid Ali Khamenei kumewaathiri kwa kina wasanii wa Iran, jambo lililoonekana katika kazi nyingi za kisanii zinazoakisi maombolezo, mapenzi na maadili aliyoyasimamia.
-
Sheikh Isa Qassim: Kiongozi Shahidi alisimama kwa ajili ya Uislamu, Umma na ubinadamu
Mwanazuoni mashuhuri wa Bahrain, Ayatullah Sheikh Isa Ahmad Qassim, amesema kuwa Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei alijitolea maisha yake kwa ajili ya Uislamu, Umma wa Kiislamu na ubinadamu, huku akieleza kuwa urithi wake utaendelea kuongoza njia ya Muqawama na umoja wa Waislamu.
-
Hilali Nyekundu: Hakuna Majeruhi Walioripotiwa Katika Hafla ya Kuaga Kiongozi Shahidi Licha ya Mamilioni ya Waombolezaji Kushiriki
Shirika la Hilali Nyekundu limetangaza kuwa hadi sasa hakuna majeruhi walioripotiwa katika hafla ya kuaga Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, licha ya mamilioni ya waombolezaji kushiriki. Shirika hilo limeeleza kuwa mafanikio hayo yametokana na usimamizi mzuri wa tukio hilo pamoja na ushirikiano wa wananchi.
-
Picha za Viatu na Koti la Kiongozi Shahidi Sayyid Ali Khamenei Zazua Mjadala Kuhusu Unyenyekevu Wake
Picha zinazoonyesha viatu na koti la Kiongozi Shahidi Sayyid Ali Khamenei zimeenea kwenye mitandao ya kijamii, huku zikitumiwa kuonyesha maisha yake ya unyenyekevu na kutopenda anasa licha ya kushika nafasi ya juu ya uongozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Burkina Faso: Iran imekuwa mfano wa kipekee wa heshima na uhuru
Waziri wa Mambo ya Nje wa Burkina Faso, Karamoko Jean Marie Traoré, amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekuwa mfano wa kipekee wa heshima, uhuru na ustahimilivu, akipongeza msimamo thabiti wa wananchi wa Iran katika kukabiliana na vitisho na mashinikizo visivyo halali.
-
Picha ya Kihistoria ya Mwili Mtukufu wa Kiongozi Shahidi Imam Sayyid Ali Khamenei Yashuhudiwa Jijini Tehran
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) – ABNA – limechapisha picha ya karibu zaidi ya mwili mtukufu wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Shahidi Ayatullah Mkuu Imam Sayyid Ali Khamenei (Qudsallahu Nafsahu Az-Zakiyyah), katika ukumbi wa Msikiti wa Imam Khomeini (Quds Sirruh), huku mamilioni ya watu duniani wakiendelea kuomboleza na kumuenzi kama “Imamu wa Wanyonge”.
-
Qalibaf Akutana na Spika wa Bunge la Iraq Pembeni ya Shughuli za Maombolezo Tehran
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amekutana na Spika wa Bunge la Iraq, Heibat Al-Halbousi, aliyefika Tehran akiwa na ujumbe wa wabunge kushiriki katika shughuli za maombolezo na kuaga kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Ujumbe wa Wanazuoni wa Palestina Wawasili Iran Kutoa Heshima kwa Mwili Msafi wa Shahidi aliyeishi kwa kutetea Quds na Watu wa Palestina
Ujumbe wa masheikh na wanazuoni kutoka Palestina umewasili Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa ajili ya kutoa heshima na kuonesha mshikamano wao kwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Kiongozi Mkuu wa Iran Shahidi Sayyid Ali Khamenei (ra); huku ukisisitiza nafasi ya Kiongozi huyo wa Mapinduzi ya Kiislamu katika kuunga mkono Quds Tukufu na haki za wananchi wa Palestina.
-
Watafiti wa Yemen na Bahrain: Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Umma Yatakuwa Tukio Kubwa Linalovuka Mipaka ya Ulimwengu wa Kiislamu
Katika mkutano maalumu ulioandaliwa na Shirika la Habari la ABNA kwa anuani ya "Urithi wa Kimkakati na Kistaarabu wa Kiongozi Shahidi wa Umma", watafiti kutoka Yemen na Bahrain walieleza kuwa mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu yatakuwa tukio la kihistoria litakalovutia hisia za ulimwengu mzima na kuleta athari kubwa za kitamaduni na kisiasa.
-
Siku Tano Zasalia kwa Kuaga Mwili wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Shahidi, Imam Sayyid Ali Khamenei
Kamati ya maandalizi ya mazishi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Shahidi, Imam Sayyid Ali Khamenei (q.s), imetangaza kuwa zimebaki siku tano pekee kabla ya kufanyika kwa hafla ya mwisho ya kuuaga mwili wa kiongozi huyo, aliyesimama kidete kupinga mfumo wa dhulma wa kikanda kwa msaada wa Muqawama.
-
Picha ya Shahidi Seyyed Kamal Kharazi Yaongezwa katika Ubao wa Kumbukumbu wa Mashahidi wa Shirika la Habari la IRNA
Kwa uwepo wa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Habari la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (IRNA), picha ya Shahidi Seyyed Kamal Kharazi imeongezwa katika ubao wa kumbukumbu wa mashahidi wa shirika hilo, ikifungua ukurasa mpya wa historia ya kujitolea na uzalendo wa wanahabari wa Iran.
-
Iraq Yajitayarisha kwa Mazishi ya Kihistoria na ya Mamilioni ya Waombolezaji kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, kufuatia kuuawa shahidi kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Imam Sayyid Ali Khamenei, na kutokana na maombi ya mara kwa mara ya wanazuoni, viongozi wa makabila na wasomi wa Iraq, miji mitakatifu ya Najaf na Karbala inajiandaa kupokea mamilioni ya waombolezaji katika mazishi ya kihistoria yatakayofanyika tarehe 8 Julai.
-
Mamilioni ya Wairaq Kuitikia Wito wa Kushiriki Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi
Takribani Wairaq milioni moja wanatarajiwa kushiriki mazishi ya kiongozi shahidi wa Mapinduzi, huku zaidi ya nusu milioni wakitarajiwa kuingia Iran kupitia mpaka wa Mehran kuelekea Tehran, Qum na Mashhad kwa ajili ya maombolezo.
-
Sayyid Ammar al-Hakim na Ayatullah Ramadhani Wajadili Uimara wa Iran na Mchakato wa Kuunda Serikali Mpya Iraq
Katika mkutano uliofanyika Baghdad, Sayyid Ammar al-Hakim na Ayatollah Reza Ramezani walijadili maendeleo ya kisiasa nchini Iraq, huku wakisisitiza uimara wa wananchi wa Iran na umuhimu wa uongozi katika kipindi cha changamoto.