Sayyid Ali Khamenei
-
Sayyid Khamenei: Kiongozi Aliyesimama Kidete Dhidi ya Ubeberu wa Kimataifa
Baada ya hatua thabiti na za kishujaa za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran dhidi ya kambi za kijeshi za Israel na Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati, dunia iliamka asubuhi ikiwa inazungumzia wasifu mpya wa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatollah Sayyid Ali Khamenei—kiongozi wa kiroho aliyeonesha ujasiri, busara na msimamo usiotetereka mbele ya madola ya kibeberu.
-
Ayatullah Khamenei:Mazungumzo na Waandamanaji Halali Yapokelewe na Kusikilizwa, Wachochezi wa Fujo na Ghasia Hawastahili Kusikilizwa Bali Wadhibitiwe
Ayatullah Khamenei amesisitiza utayari wa mazungumzo na waandamanaji halali, huku akionya kuwa wachochezi wa fujo—aliowataja kuwa mamluki wa adui—hawastahili mazungumzo na wanapaswa kuzuiwa kwa sababu ya kueneza kauli mbiu dhidi ya Uislamu, Iran na Jamhuri ya Kiislamu.
-
Vitisho vya Trump dhidi ya Iran Vinatokana na Kukata Tamaa: IRGC
IRGC imesema vitisho vya Rais wa Marekani Donald Trump dhidi ya Iran vinatokana na kukata tamaa baada ya kushindwa kuishinikiza Iran, ikisisitiza utii wake kwa Kiongozi wa Mapinduzi Ayatollah Ali Khamenei na kuendelea kulinda taifa la Iran na kuimarisha njia ya Shahidi Qassem Soleimani katika Mhimili wa Upinzani.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Tasnia ya Madahi inapaswa kuwa kitovu cha fasihi ya Muqawama na ufafanuzi wa mafundisho ya dini na mapinduzi
Katika hotuba yake iliyochukua takriban saa tatu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei aliwapongeza Wairani kwa kuadhimisha kuzaliwa kwa Bibi Fatimah (a.s) na kusema kuwa “mwananchi wa Iran, kwa kupitia msimamo wa kitaifa wa kimapinduzi, ameshindwa kabisa njama za adui kutaka kubadilisha utambulisho wa kidini, kihistoria na kiutamaduni wa taifa hili.”
-
Tone kutoka Nahjul-Balagha 27 | Kuheshimu Hadhi ya Imamu ni Nini?
Matokeo ya utiifu ni nini?. Amirul-Mu’minin Ali bin Abi Talib (AS) katika khutba ya 156 anasema: «إِنْ أَطَعْتُمُونِی فَإِنِّی حَامِلُکُمْ إِنْ شَاءَ اللَّهُ عَلَی سَبِیلِ الْجَنَّةِ» Yaani: “Mkinitii mimi – mimi kama Imamu– bila shaka nitawaongoza katika njia ya Peponi"
-
Imam Khamenei: Uhasama kati ya Iran na Marekani ni wa asili, ni mgongano wa maslahi kati ya mitindo miwili
Hivi karibuni kabla ya tarehe 4 Novemba, inayojulikana kama “Siku ya Wanafunzi na Siku ya Kitaifa ya Kupambana na Ukorofi wa Kidunia”, Imam Khamenei, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, alikutana na wanafunzi wa rika zote, wakiwemo wanafunzi wa vyuo vikuu, pamoja na familia za mashahidi wa Vita vya Siku 12 Vilivyowekezwa"
-
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu:“Wazayuni hawakutarajia nguvu ya makombora ya Iran / Marekani haina haki kujihusisha na teknolojia ya Iran"
Ayatollah Sayyid Ali Khamenei amebainisha kwamba: Marekani haina haki kujihusisha na suala la teknolojia ya nyuklia ya Iran - na akahoji kuhusiana na Trump akisema: Wewe ni nani hasa?”.
-
Chuo cha Al-Mustafa (s) - Tanzania Kimeandaa Kongamano la Kielimu Kuhusu Ustaarabu wa Magharibi na Mikakati yake ya Kikoloni
Ustaarabu wa Magharibi na misingi ya kuuelewa ipasavyo.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ameipongeza timu ya taifa ya Iran ya mieleka ya Greco-Roman kwa ushindi wao wa ubingwa wa dunia
Hii ni mara ya kwanza katika historia ya michezo ya nchi yetu ambapo Timu ya Taifa ya mieleka ya “freestyle” na “Greco-Roman” zimefanikiwa kwa pamoja kutwaa ubingwa wa dunia katika mashindano moja.
-
Kiongozi wa Mapinduzi Katika Mkutano na wanachama wa Serikali:
"Tuweke roho ya Kazi na Juhudi juu ya hali ya Kutokuwa Vitani wala kuwa na Amani (Hali ya 'si vita, si amani')
Ayatollah Khamenei katika kikao na Rais pamoja na Baraza la Mawaziri alisisitiza juu ya umuhimu wa 'kutawala kwa hali ya kazi, juhudi na matumaini' dhidi ya 'hali ya si vita wala amani'
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ataka Utekelezaji wa Makubaliano ya Kistratejia kati ya Iran na China
Ayatollah Khamenei amesisitiza nafasi ya kihistoria na ya kimkakati ya Iran na China katika bara la Asia na duniani, na akasema kuwa: "Iran na China, zikiwa na historia ya ustaarabu wa kale katika pande mbili za Asia, zina uwezo wa kuleta mabadiliko katika medani ya kimataifa na kikanda. Kuweka katika vitendo vipengele vyote vya makubaliano ya kistratejia, kutarahisisha njia hii."
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu atoa rambirambi kufuatia kifo cha Msanii wa Kiirani Mahmoud Farshchian: "Ameacha nyuma kazi za sanaa zisizofutika"
"Msanii mashuhuri na maarufu, Bwana Mahmoud Farshchian, alikuwa nyota angavu katika anga ya sanaa ya Kiirani. Uaminifu wake na ucha Mungu wake vilimuwezesha kuutumia uwezo wake wa kipekee katika kuhudumia maarifa na mambo ya kidini, na ameacha nyuma kazi za sanaa zisizofutika. Rehema na radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake. Nawasilisha rambirambi za dhati kwa familia yake, marafiki zake, wanafunzi wake, na jamii ya wasanii nchini."
-
Katika Kumbukizi ya Imam Reza (a.s): Kiongozi Mkuu Atoa Wito wa Kulinda Umoja na Kukemea Jinai za Kizayuni
Ayatollah Khamenei: "Marekani Haitaki Iran Isimame Imara, Bali Itii Amri Zake".
-
Sayyid Ali Khamenei: "Utawala wa Kizayuni haukufikiria kamwe kupokea mashambulizi kama haya kutoka kwa Jamhuri ya Kiislamu".
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu - Leo akihutubia Taifa la Iran, ametoa ufafanuzi mzuri mno wa matukio yalivyojiri, na kauli imara za kutia moyo kwa wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, ambazo kwa hakika zimeonyesha mshikamano wa kitaifa, ujasiri, na kukataa kuachia madikteta au nguvu za kigeni na kibeberu kutawala na kuidhibiti Kijeshi Mashariki ya Kati. Pia, kauli za Kiongozi huyu imara na mwenye busara na hekima ya hali ya juu, zinaonyesha msimamo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kukabiliana na mashambulizi ya nje, na kutotetereka katika suala zima la kuifyekelea mbali mikono ya adui yeyote yenye nia ovu dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Imamu wa Ijumaa wa Baghdad: Waislamu wote wanapaswa kusimama na Ayatollah Khamenei
Imamu wa Ijumaa wa Baghdad ametoa taarifa yenye maneno makali kufuatia jinai ya hovyo ya Trump.