Baadhi ya watu wanaikimbia dini kwa kusema: Tunapenda kuwa sisi wenyewe. Hatupendi kuambiwa tufanye nini au nini tusifanye. Tunataka kuwa huru.
Jibu letu kwa marafiki hawa ni kwamba, dini inataka kitu kimoja kutoka kwako pia. Dini pia inataka uwe mwenyewe na usijisahau.
Kama Qur’ani inavyosema:
«.وَلَا تَكُونُواْ كَٱلَّذِينَ نَسُواْ ٱللَّهَ فَأَنسَىٰهُمۡ أَنفُسَهُمۡ»
Wala msiwe kama wale walio msahau Mwenyezi Mungu, na Yeye akawasahaulisha nafsi zao. (Hashr/19)
ina maana gani? Ina maana kuna uhusiano wa ajabu kati ya kujisahau na kumsahau Mungu. Ina maana kwamba ukitaka kuwa wewe mwenyewe, lazima uwe na Mungu, vinginevyo utajisahau.
Na jambo linalopaswa kutiliwa maanani ni kwamba kujisahau kunamaanisha kusahau ubinadamu na kuwa mja wa Mungu, na kusahau ubinadamu kunamaanisha mwanzo wa ubaya.
Chanzo: alanwaralmunirah