28 Machi 2025 - 17:41
Source: Parstoday
Zainab Nasrullah: Kuwauwa viongozi wa Muqawama hakutadhoofisha mapambano

Binti wa Shahidi Sayyid Hassan Nasrullah, aliyekuwa Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa kuwauwa viongozi wa Muqawama hakutadhoofisha mapambano ya ukombozi.

Zainab Nasrullah, ambaye alikuwa akizungumza leo kabla ya hotuba ya Swala ya Ijumaa ya mjini Tehran amesema mbele ya umati wa watu waliohudhuria ibada hiyo sambamba na maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Quds kwamba: Tunaahidi mbele ya Mwenyezi Mungu, Imam wetu wa Zama, marehemu Imam Khomeini (M.A) na shahidi wetu Sayyid Hassan Nasrullah, kwamba tutaendeleza njia ya Muqawama na kuikamilisha njia hii, hata kama sisi sote tutakufa shahidi. 

Binti wa Katibu wa zamani Hizbullah ya Lebanon ameashiria matamshi ya Sayyid Hassan Nasrullah na kusema: Sayyid shahidi wetu mara kadhaa alitilia mkazo nukta kwamba "Lebanon haitakuwa katika mikono ya Israel abadani", kwa hiyo msidanganywe na kumwagwa damu zetu, kwa sababu damu hizi daima zimekuwa washindi na zitaendelea kushinda siku zote; Na tunaamini ahadi na nusra ya Mwenyezi Mungu."

342/

Your Comment

You are replying to: .
captcha