Kulingana na Shirika la Habari la ABNA likinukuu CNN, Rais wa utawala wa Kizayuni, Isaac Herzog, alijibu makubaliano ya Gaza, lakini bila kutaja uhalifu wa utawala huo dhidi ya watu waliodhulumiwa katika Ukanda huo, alidai kwa ishara ya kujipendekeza kwa umma: "Moyo wa Israeli unapiga pamoja na mateka na familia zao!"
Rais wa utawala wa Kizayuni alidai: "Ninaelezea unga mkono wangu kamili kwa makubaliano yaliyofikiwa. Ninamshukuru Rais Trump kwa usimamizi wake katika kuhakikisha uhuru wa mateka na kukomesha vita."
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu Hamas ilitangaza katika taarifa saa chache zilizopita: "Tunatangaza kufikiwa kwa makubaliano yanayopelekea kumalizika kwa vita huko Gaza, kujitoa kwa vikosi vya uvamizi [vya Kizayuni], kuingia kwa misaada [ya kibinadamu], na kubadilishana mateka."
Hamas pia ilitoa wito kwa Trump, nchi za upatanishi, na pande za Kiarabu na Kiislamu kumlazimisha wavamizi wa Kizayuni kutekeleza kikamilifu makubaliano hayo.
Your Comment