Kulingana na shirika la habari la Abna, likinukuu Reuters, Msalaba Mwekundu, ambao uliwasili dakika chache zilizopita katika eneo la hatua ya pili ya kuachiliwa kwa wafungwa wa Kizayuni huko Khan Yunis, unawapokea wafungwa waliosalia.
Operesheni hii ilianza dakika chache zilizopita kusini mwa Ukanda wa Gaza.
Vyanzo vya habari vya utawala wa Kizayuni viliripoti kwamba Msalaba Mwekundu umepokea baadhi ya wafungwa hawa na kwamba wako njiani kuelekea maeneo yaliyokaliwa. Kituo cha Al Mayadeen pia kilinukuu vyombo vya habari vya Kiebrania vikisema kwamba Msalaba Mwekundu umepokea wafungwa 13 wa Kizayuni. Kwa hivyo, vikosi vya upinzani vya Palestina vimekashikabidhi wafungwa 20 hai wa utawala wa Kizayuni.
Your Comment