18 Desemba 2014 - 18:12
Rais wa zamani wa Marekani amsifu Obama kwa kurejesha uhusinao na Cuba

Rais wa zamani wa Marekani Jimmy Carter amesema anajisikia mwenye furaha kwa juhudi za rais Obama kurejesha uhusiano wa kidiplomasia na Cuba.

Rais  wa  zamani  wa  Marekani Jimmy Carter  amesema  anajisikia mwenye  furaha  kwa  juhudi  za  rais Obama kurejesha  uhusiano wa  kidiplomasia  na  Cuba. Carter ameiita  hatua  hiyo  ya mabadiliko  ya  sera  kuwa  ya  kishupavu. Carter  anapuuzia shutuma  kuwa  rais Barack Obama  anawafurahisha  viongozi  wa kikomunist  wa  Cuba., kama  anavyosema  seneta  wa  chama  cha Republican Marco Rubio.

Amesema leo  kuwa  njia  sahihi  ya  kuleta  demokrasia  kwa Wacuba  ni  kuwaruhusu  Wamarekani  kwenda  nchini  humo kufanya  biashara  na  kuwekeza.

Carter  alijaribu  kurejesha  uhusiano  na  Cuba  muda  mfupi baada ya  kuingia  madarakani  mwaka 1977, kwa  kuanzisha  ubalozi  wa Marekani  na  kujadili kuachiliwa  huru  kwa  maelfu  ya  wafungwa.

Wakati  huo  huo  kiongozi  wa  kanisa  Katoliki  Papa  Francis amesifu  hatua  ndogo  za  kidiplomasia  zinazofikiwa  ambazo zimeleta  mahusiano  bora  kati  ya  Marekani  na  Cuba.

Tags