Venezuela
-
Mkuu wa Usalama wa Ikulu wa Venezuela Afukuzwa / Na Kukamatwa kwa Tuhuma za Usaliti
Taarifa za kina kuhusu kinachoendelea Nchini Venezuela bado zinaendelea kutokea, na hali ya kisiasa nchini Venezuela iko wazi kwa mfululizo wa taarifa mpya zinazotoka zikitoa ufafanuzi wa kina juu ya kilichotokea kuhusiana na kusalitiwa na kutekwa kwa Rais wa Nchi hiyo.
-
Marekani Yatwaa Meli ya Mafuta ya Kirusi Iliyo Husiana na Mafuta ya Venezuela
Hali hii inachangia kuongeza mvutano wa kimataifa, huku washirika wa Venezuela na Urusi wakionya kuhusu matokeo yanayoweza kutokea kutokana na hatua hizo za Marekani.
-
Washington Yakanusha Kutuma Maafisa wa Kijeshi nchini Venezuela
Mike Johnson, Spika wa Bunge la Marekani, amekana Kutumwa kwa Maafisa wa Kijeshi Kwenda Venezuela. Mike Johnson, spika wa Bunge la Marekani, ameweka wazi kuwa Marekani haijasambaza au kutuma majeshi yake nchini Venezuela.
-
Rais wa Baraza la Wahdat Muslimin Pakistan:
Ayatollah Khamenei amewashinda maadui katika kila vita / Wafuasi wa Imam Hussein (a.s) daima wamesimama dhidi ya dhuluma
"Kilichotokea Venezuela ni cha kusikitisha; waziri mkuu wetu amempendekeza mtu apate Tuzo ya Nobel ilhali alihusika katika utekaji nyara wa rais aliyechaguliwa wa nchi hiyo na familia yake. Viongozi wa Pakistan wanapaswa kulaani vikali hatua za Donald Trump. Trump hata alivunja katiba ya nchi yake mwenyewe.”
-
Rais wa Cuba: Mataifa ya Amerika ya Kusini Lazima Yaungane
Rais wa Cuba ametoa wito kwa mataifa ya Amerika ya Kusini kuimarisha umoja wao kufuatia operesheni ya kijeshi ya Marekani iliyosababisha kukamatwa kwa Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro, akitaja hatua hiyo kuwa ni “shambulio la kinyama” dhidi ya taifa huru.
-
Trump Atangaza Kukamatwa kwa Rais wa Venezuela Nicolás Maduro katika Operesheni Maalum
Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kukamatwa kwa Rais wa Venezuela Nicolás Maduro na mkewe katika operesheni maalum, akisema walihamishiwa New York kukabili mashtaka ya jinai, huku akisisitiza kuwa Marekani itaendelea kuhusika katika mustakabali wa Venezuela na kupambana na biashara ya dawa za kulevya.
-
Kuanzia Panama 1989 hadi Venezuela 2025; Kurudiwa kwa Sera ya Uingiliaji wa Marekani katika Amerika ya Kusini
Uingiliaji huu, ambao mara nyingi umelaaniwa na jumuiya ya kimataifa, umezaa matokeo ya kudumu kama vile ukosefu wa utulivu, ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na kudhoofishwa kwa uhuru wa mataifa - hali inayosisitiza tena umuhimu wa kuheshimu sheria za kimataifa na kupinga sera za upande mmoja zinazoathiri amani ya kikanda.
-
Venezuela yaamuru Jeshi la Wanamaji kuandamana na meli za mafuta katikati ya mzingiro wa baharini wa Marekani
Rais wa Venezuela Nicolás Maduro ameagiza jeshi la wanamaji kuandamana na meli zinazobeba mafuta ghafi ya Venezuela kuelekea masoko ya Asia, ikiwa ni hatua ya moja kwa moja ya kujibu kile ambacho Caracas inakiita mzingiro wa baharini uliowekwa na Marekani chini ya Rais Donald Trump.
-
Ubalozi wa Iran: Hatua ya Marekani dhidi ya Venezuela ni wizi katika Bahari ya Karibi
Ubalozi wa Iran mjini Caracas, huku ukilaani vikali kitendo cha Marekani cha kukamata mafuta kwenye eneo la karibu na pwani ya Venezuela, umetangaza kuwa hatua hiyo ya Marekani ya kukamata meli ya mafuta ya Venezuela bila sababu yoyote ya kisheria ni ukiukwaji mkubwa wa sheria na kanuni za kimataifa.
-
Mazungumzo ya Simu kati ya Trump na Maduro Katikati ya Vitisho vya Kijeshi vya Marekani Dhidi ya Venezuela
Rais wa Marekani, Donald Trump, alifanya mawasiliano ya simu na mwenzake wa Venezuela, Nicolás Maduro, na wakajadili uwezekano wa kufanyika kwa mkutano wa ana kwa ana huko Washington, kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa na New York Times. Mawasiliano haya yalifanyika wakati mvutano ukiwa umeongezeka kufuatia hatua ya Marekani kupeleka majeshi yake katika eneo la Karibi na tuhuma za ulanguzi wa dawa za kulevya dhidi ya Maduro-tuhuma ambazo Venezuela huziona kama kisingizio cha kuandaa mabadiliko ya serikali.
-
Trump: Hivi karibuni tutaanzisha operesheni ya kijeshi ya ardhini nchini Venezuela
Rais wa Marekani ametangaza kuongezwa kwa mashambulizi kutoka baharini hadi ndani ya ardhi ya Venezuela, na kusema kuwa Washington “hivi karibuni sana” italenga njia za ardhini zinazotumiwa kwa magendo.
-
Maduro: "Trump ameongeza umoja wa kitaifa nchini Venezuela"
Rais wa Venezuela amesema: Tuhuma zisizo na msingi za Trump dhidi ya Venezuela zimeongeza umoja na mshikamano wa watu na serikali ya Venezuela.
-
Mkusanyiko wa watu wa Venezuela katika kuunga mkono malengo ya Palestina na kulaani mauaji ya kimbari yanayoendelea Gaza
Katika jimbo la Vargas, Venezuela, vikundi na mashirika ya kijamii, kwa msaada wa "Jukwaa la Mshikamano na Malengo ya Palestina", siku ya Jumamosi tarehe 13 Septemba 2025, walikusanyika pamoja ili: Kulaani mauaji ya kimbari yanayoendelea Gaza, Kuonesha upinzani wao dhidi ya sera na vitisho vya serikali ya Marekani dhidi ya nchi yao, Na kusisitiza juu ya haki ya Venezuela ya kujitawala kama taifa.
-
Maduro: Mamilioni ya Wavenezuela wako tayari kwa vita na kukabiliana na wavamizi wa Kimarekani
Rais wa Venezuela, huku akilaani shambulio la utawala wa Kizayuni dhidi ya Qatar, ametangaza kuwa wananchi wa nchi hiyo wako tayari kwa vita dhidi ya wavamizi wa Marekani.
-
(Radi amali) Mwitikio wa Maduro kwa Kupelekwa kwa Manowari za Marekani Venezuela
Rais wa Venezuela ameikosoa hatua ya Marekani ya kupeleka manowari tatu za kivita karibu na pwani ya nchi yake, akitaja kitendo hicho kuwa ni “uvamizi wa kigaidi wa kijeshi, usio halali na kinyume cha sheria.”
-
Venezuela: Dunia imefurahishwa na pigo Kali la Iran dhidi ya Utawala wa Kizayuni
Waziri Mkuu wa Venezuela l: "Venezuela inasimama bega kwa bega na Iran katika Haki yake ya kujihami na kuilinda amani yake dhidi ya majaribio yoyote ya jinai za kizayuni".
-
Rais wa Baraza la Wawakilishi la Iran Awasilisha Zawadi ya Familia ya Shahidi Soleimani kwa Rais Maduro wakati wa Ziara Caracas
Rais wa Bunge | Baraza la wawakilishi la Iran akutana na Rais Maduro Caracas, na kumkabidhi sanamu ya Jenerali Shahidi Qasem Soleimani, iliyotumwa na familia ya Shahidi Soleimani kama zawadi.