Venezuela
-
Mazungumzo ya Simu kati ya Trump na Maduro Katikati ya Vitisho vya Kijeshi vya Marekani Dhidi ya Venezuela
Rais wa Marekani, Donald Trump, alifanya mawasiliano ya simu na mwenzake wa Venezuela, Nicolás Maduro, na wakajadili uwezekano wa kufanyika kwa mkutano wa ana kwa ana huko Washington, kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa na New York Times. Mawasiliano haya yalifanyika wakati mvutano ukiwa umeongezeka kufuatia hatua ya Marekani kupeleka majeshi yake katika eneo la Karibi na tuhuma za ulanguzi wa dawa za kulevya dhidi ya Maduro-tuhuma ambazo Venezuela huziona kama kisingizio cha kuandaa mabadiliko ya serikali.
-
Trump: Hivi karibuni tutaanzisha operesheni ya kijeshi ya ardhini nchini Venezuela
Rais wa Marekani ametangaza kuongezwa kwa mashambulizi kutoka baharini hadi ndani ya ardhi ya Venezuela, na kusema kuwa Washington “hivi karibuni sana” italenga njia za ardhini zinazotumiwa kwa magendo.
-
Maduro: "Trump ameongeza umoja wa kitaifa nchini Venezuela"
Rais wa Venezuela amesema: Tuhuma zisizo na msingi za Trump dhidi ya Venezuela zimeongeza umoja na mshikamano wa watu na serikali ya Venezuela.
-
Mkusanyiko wa watu wa Venezuela katika kuunga mkono malengo ya Palestina na kulaani mauaji ya kimbari yanayoendelea Gaza
Katika jimbo la Vargas, Venezuela, vikundi na mashirika ya kijamii, kwa msaada wa "Jukwaa la Mshikamano na Malengo ya Palestina", siku ya Jumamosi tarehe 13 Septemba 2025, walikusanyika pamoja ili: Kulaani mauaji ya kimbari yanayoendelea Gaza, Kuonesha upinzani wao dhidi ya sera na vitisho vya serikali ya Marekani dhidi ya nchi yao, Na kusisitiza juu ya haki ya Venezuela ya kujitawala kama taifa.
-
Maduro: Mamilioni ya Wavenezuela wako tayari kwa vita na kukabiliana na wavamizi wa Kimarekani
Rais wa Venezuela, huku akilaani shambulio la utawala wa Kizayuni dhidi ya Qatar, ametangaza kuwa wananchi wa nchi hiyo wako tayari kwa vita dhidi ya wavamizi wa Marekani.
-
(Radi amali) Mwitikio wa Maduro kwa Kupelekwa kwa Manowari za Marekani Venezuela
Rais wa Venezuela ameikosoa hatua ya Marekani ya kupeleka manowari tatu za kivita karibu na pwani ya nchi yake, akitaja kitendo hicho kuwa ni “uvamizi wa kigaidi wa kijeshi, usio halali na kinyume cha sheria.”
-
Venezuela: Dunia imefurahishwa na pigo Kali la Iran dhidi ya Utawala wa Kizayuni
Waziri Mkuu wa Venezuela l: "Venezuela inasimama bega kwa bega na Iran katika Haki yake ya kujihami na kuilinda amani yake dhidi ya majaribio yoyote ya jinai za kizayuni".
-
Rais wa Baraza la Wawakilishi la Iran Awasilisha Zawadi ya Familia ya Shahidi Soleimani kwa Rais Maduro wakati wa Ziara Caracas
Rais wa Bunge | Baraza la wawakilishi la Iran akutana na Rais Maduro Caracas, na kumkabidhi sanamu ya Jenerali Shahidi Qasem Soleimani, iliyotumwa na familia ya Shahidi Soleimani kama zawadi.