Ikumbukwe kuwa nchini Ufaransa na Hispania kuna maandamano wananchi wanapinga serikali zao lakini hakuna nchi yeyote ya Ulaya iliyounga mkono wapinzani au hata kuwapelekea silaha wananachi ili waziangushe serikali zao.
Waziri wa ulinzi wa Venezuela Vladmir Padrino amesisitiza kwamba jeshi nchini humo litaendelea kuimarisha hali ya tahadhari dhidi ya ukiukwaji wowote kwenye mipaka yake na kwamba linaendelea kumtii Maduro ambaye ni ras Halali kikatiba.