Makala
-
Makala Fupi Kuhusu Kuzaliwa kwa Sayyidat Fatima Maasoumeh (sa) | Imam Ridha (as) alisema: "Yeyote atakayemzuru Fatima Maasoumeh Qom, atapata Pepo."
Fatima Maasoumeh (sa) alikuwa mashuhuri kwa elimu yake, ibada, na ufasaha. Alifuatilia harakati za kaka yake, Imam Ridha (as), na alikuwa mstari wa mbele katika kutetea haki na kufichua dhulma za watawala wa wakati huo. Katika safari yake ya kuelekea Khurasan kumtembelea kaka yake aliyehamishwa kwa nguvu na Khalifa Ma’mun, Sayyidat Fatima alifika mji wa Qom (Iran ya leo), ambako alipata maradhi mazito na kufariki dunia tarehe 10 Rabi'ul Thani mwaka 201 Hijria. Alizikwa mjini Qom, ambao baadaye ukawa kituo muhimu cha elimu ya Kiislamu.
-
Matendo Mema katika Dua na Swala za Sunna (Sehemu ya 1)
Huu ni mkusanyiko uliokusanya baadhi ya matendo ya kufanya usiku na mchana, swala za Sunnah zilizopokewa, ponyo, kinga, dhikir, dua za ajabu, athari za baadhi ya Aya na ufupisho wa kuwafanyia adabu waliokufa, nimezikusanya ili niziambatanishe kwenye Mafatihul Jinani kisha kitabu kikamilike kwa njia zote na iwe na manufaa kwayo yaliyotimia.
-
Siku ya Wakati Maalum:
Ni ipi Maana ya Kauli ya Mwenyezi Mungu aliposema kumwambia Shetani: "یوم الوقت المعلوم" “Siku ya Wakati Maalum"
katika ufahamu wa Shia (Wafuasi wa Ahlul-Bayt - a.s - ), "یوم الوقت المعلوم" ni Siku ya dhahiri ya Haki na Uadilifu wa Mwenyezi Mungu Duniani, yaani Siku ya Mapinduzi ya Dunia yakiongozwa na Imam Mahdi (a.t.f.s), kabla ya Siku ya Kiyama.
-
Hadithi ya Shetani na Mwanadamu:
"Siri ya Muda wa Shetani Kuishi: Kwa Nini Mwenyezi Mungu Alimpa Shetani Muda Mrefu wa Kuishi?
Tangu wakati huo ambapo Shetani aliasi na kukataa kumsujudia Adam (a.s), mzozo wa kihistoria kati yake na Mwanadamu ulianza; mzozo ambao unaendelea hadi leo hii. Lakini swali muhimu ni hili: Kwa nini Mwenyezi Mungu alimpa adui huyu katili (Shetani) muda mrefu wa kuendelea kuishi na kujaribu na kuwapoteza watoto wa Adam (Wanadamu)?!. Nakuletea Hadithi nzuri na yenye mazingitio ndani yake kuhusu Shetani na Mwanadamu, na utaijua sababu na siri ya Ruhusa ya Mwenyezi Mungu kwa Shetani ili aendelee kuishi kwa muda mrefu.
-
Tarehe 25 Shawwal Mwaka 148 Hijiria, ulimwengu wa Kiislamu ulipatwa na Huzuni kufuatia kuondokewa na mmoja wa Ahlul-Bayti wa Mtume wa Uislamu (saww)
Licha ya kwamba Ahlul-Bayti wa Mtume (s.a.w.w) walikabiliwa na changamoto tofauti kisiasa na kijamii, lakini walijitahidi kuhakikisha wanainua bendera ya dini ya Kiislamu katika zama zao zote. Dakta Shahid Mutwahhari, mwanafikra mashuhuri wa Iran anaandika kwa kusema: " Ahlul-Bayti (a.s) walikuwa wakichunga maslahi ya Kiislamu na Waislamu kwa ujumla".
-
Jinsi ya kuthibitisha Isma ya Maimamu 9 (a.s) kutoka ndani ya Qur’an Tukufu
“Na (Kumbukeni) Ibrahim alipojaribiwa na Mola wake kwa matamko, naye akayatimiza. Akasema: Hakika mimi nitakufanya kuwa Imam wa watu. Ibrahim akasema: Je,na Kizazi changu (pia)?.(Ndiyo, lakini) ahadi yangu haiwafikii Madhalimu.”
-
Fiqh Na Hukumu Zake:
Namna ya Kutoharisha vitu vilivyo najisika kwa kutumia Maji
Anuani ya makala yetu inasema: "Kwa kutumia Maji" kwa kuwa maji ndio yaliyochukua nafasi kubwa katika kutoharisha vilivyonajisika kuliko vingine vyote vyenye kutoharisha.Tutamia herufi (S) kuashiria swali na herufi (J) kuashiria jibu lake.
-
Njia ya Dhambi Huanza na Dakika ya Uzembe
Tunamuomba Mwenyezi Mungu atujaalie sote tupate taufiki ya kushikamana na Ahlul-Bayt (a.s) wa Mtume Muhammad (s.a.w.w), kwani wao ndio Njia iliyonyooka, na atakayeshikamana nao wao na Qur'an Tukufu, huyo ataepukana na upotevu, kwa sababu wao ndio sehemu ya Kizito cha pili baada ya Qur'an Tukufu, na Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w) ametuusia katika Hadithi Sahih na Mutawatiri ya Thaqalayni, kushikamana na Ahlul-Bayt (a.s) na Quran Tukufu ili tuje kupotea baada yake.
-
Wa Kwanza Kuitwa Amirul-Muuminina:
Mwenyezi Mungu (s.w.t) Alimpa Ali bin Abi Talib Lakabu ya “Amirul Muuminina”
Ukufungua kurasa za Historia ya Maisha yake safi ya Imam Ali bin Abi Talb (a.s), utamkuta kwamba yeye ni wa mwanzo katika kila kitu, kisha wengine wanafuata nyuma yake katika kitu hicho.
-
Ushahidi wa Mawalii Katika Kumfananisha Ali na Manabii
Ali (a.s), wapo Watu waliodai kuwa wanampenda, mpaka wakamfanya kuwa ni mungu, ametakasika Mwenyezi Mungu na wanayo mshirikisha nayo. Na wapo watu waliomchukia na wakampiga vita, wakamtukana na kumlaani, wakakufuru na wakatoka katika Uislamu. Na wapo baadhi ya Watu waliompenda, wakawa watiifu kwake, na wakashikamana naye kama alivyoamrisha Mtume (s.a.w.w), basi kwa hakika hao ndio waumini wa kweli.