Main Title
31 Machi 2024
Jeshi la Iran laapa kulinda usalama na uhuru wa nchi
Vikosi vya Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vimetangaza azma ya kuendeleza juhudi za kiwango cha juu ili kufikia malengo ya Mapinduzi ya Kiislamu na kulinda usalama na uhuru wa taifa.
31 Machi 2024
Jihad Islami: Wapalestina hawangeweza kusimama dhidi ya Israel bila ya kuungwa mkono na Iran
Kiongozi mkuu wa Harakati ya Jihad Islami ya Palestina ametangaza bayana kuwa watu wa Palestina hawangeweza kusimama dhidi ya utawala haramu wa Israel kama kusingekuwa na uungaji mkono kamili wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
31 Machi 2024
Maadhimisho ya YaumuLlah, Siku ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
YaumuLlah ya tarehe 12 Farvardin mwaka 1358 Hijria Shamsia (iliyosadifiana na Aprili Mosi, 1979), yenye maana ya Siku ya Mwenyezi Mungu, si siku rasmi tu katika kalenda ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, bali ni siku kubwa pia kwa wanyonge duniani na kwa harakati za ukombozi pamoja na mataifa yanayopambana na dhulma, uistikbari na ukoloni.
31 Machi 2024
Mkurugenzi Mkuu wa IAEA: Iran haina silaha za nyuklia
Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia (IAEA) ametenganisha baina ya kategoria ya kurutubisha madini ya urani na mchakato wa uundaji silaha za nyuklia na kutangaza kuwa Iran haitengenezi silaha za nyuklia licha ya kuwa na akiba ya urani iliyorutubishwa.
31 Machi 2024
Kwa mnasaba wa "Siku ya Ardhi", HAMAS yautolea wito Umma wa Kiislamu kuikomboa Palestina
Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetoa taarifa maalumu kwa mnasaba wa "Siku ya Ardhi" ikisisitiza kuwa kuikomboa ardhi ya Palestina na matakatifu yake ni jukumu la Umma wote wa Kiislamu.
31 Machi 2024
61% ya Waisraeli hawaamini kama vita vya Ghaza vitamalizika kwa kusambaratishwa HAMAS
Matokeo ya uchunguzi wa maoni uliofanywa Palestina inayokaliwa kwa mabavu iliyopandikizwa jina bandia la Israel yanaonyesha kuwa asilimia 61 ya Wazayuni hawaamini kama vita vya Ghaza vitamalizika kwa "kusambaratishwa harakati ya Hamas".
31 Machi 2024
Licha ya kuikosoa Israel hadharani, Biden ameidhinisha kwa siri silaha mpya za kuwaulia Wapalestina
Rais Joe Biden wa Marekani hivi karibuni ameidhinisha kwa siri kupatiwa utawala wa Kizayuni wa Israel silaha mpya za kivita zenye gharama ya mabilioni ya dola zikiwemo aina za kisasa za mabomu na ndege za kivita.
31 Machi 2024
Wapiganaji wa Muqawama Iraq washambulia kituo 'muhimu' cha kijeshi cha Israel
Kundi la Wapiganaji wa Mapambano ya Kiislamu (Muqawama) Iraq limetangaza kushambulia kituo "muhimu" cha kijeshi cha utawala wa Israel kilichoko kaskazini mwa maeneo yanayokaliwa kwa mabavu katika kuendelea kuwaunga mkono Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, ambao wanastahimili vita vya mauaji ya halaiki ya Israel.
31 Machi 2024
Wapalestina zaidi ya 400 wameuawa shahidi katika hospitali ya al Shifa iliyozingirwa
Vyombo vya habari kutoka Ukanda wa Gaza vimetangaza kuwa Wapalestina zaidi ya 400 wameuawa katika mashambulizi ya jeshi la Israel katika Hospitali ya al Shifa ambayo inaendelea kuzingirwa na utawala wa Kizayuni kwa siku ya 13 sasa.
29 Machi 2024
Kupokewa vizuri ripoti ya UN kuhusu mauaji ya kimbari yanayofanywa na Israel huko Ghaza
Tathmini ya ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya Palestina juu ya mauaji ya umati yanayofanywa na Israel kwenye Ukanda wa Ghaza imepokewa vizuri na kuungwa mkono na wawakilishi wa nchi za dunia ndani ya umoja huo.
29 Machi 2024
Erdogan: Dunia iishinikize Israel itekeleze azimio la Baraza la Usalama la UN
Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan ameitaka jamii ya kimataifa iendelee kuushinikiza utawala wa Kizayuni wa Israel utekeleze azimio la kutaka kusitishwa mara moja mapigano huko Gaza, lililopasishwa majuzi na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
29 Machi 2024
UN: Huenda Israel imetenda jinai ya kivita kwa kutumia njaa kama silaha ya vita
Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amesema hatua ya utawala wa Israel kutumia njaa kama silaha dhidi ya watu Wapalestina wa Ukanda wa Gaza yumkini ikawa jinai ya kivita.
29 Machi 2024
ICJ: Israel lazima ihakikishe msaada wa dharura, chakula vinaingizwa Ghaza bila kuchelewa
Mahakama ya Juu zaidi duniani ya Haki ICJ imeuamuru utawala wa Kizayuni wa Israel "kuhakikisha msaada wa haraka wa kibinadamu" unaingizwa huko Ghaza bila kuchelewa, ikisisitiza kuwa "njaa imeshaingia" katika eneo hilo.
29 Machi 2024
CDC: Maambukizi ya magonjwa ya zinaa yameongezeka sana Marekani
Mambukizi ya magonjwa ya zinaa (STIs) yanaonekana kuongezeka kwa kiwango cha kuogofya miongoni mwa watu wazima nchini Marekani.
29 Machi 2024
Iran: Walimwengu wana wajibu wa kuubebesha dhima utawala wa Kizayuni
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameitaka jamii ya kimataifa ichukue hatua na kuubebesha dhima utawala wa Kizayuni, baada ya Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa katika Masuala ya Palestina kufanya tathmini ambayo imezitaja jinai za utawala wa Kizayuni huko Ukanda wa Gaza kuwa ni mauaji ya kimbari.
29 Machi 2024
Kiongozi Mkuu: Ghaza ndiyo mshindi mkuu kwenye medani ya vita na utawala wa Israel mwangamizaji wa kizazi
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema vikosi vya Muqawama na watu wa Ghaza ndio washindi kwenye medani ya vita na utawala wa Israel mwangamizaji wa kizazi na akasisitiza kwa kusema: kilele cha kuheshimika na kusimama imara watu wa Ghaza na Palestina na kushindwa utawala wa Kizayuni katika vita hivyo vya miezi sita ni tukio na jambo lenye rehma za Mwenyezi Mungu.
29 Machi 2024
Spika Qalibaf: Ulimwengu wote wa Kiislamu una wajibu wa kuunga mkono Muqawama wa taifa la Palestina
Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amepongeza istikama na kusimama imara kusio na mfano kwa Muqawama na wananchi wa Palestina dhidi ya utawala ghasibu wa Israel na akasema, Ulimwengu mzima wa Kiislamu una wajibu wa kuliunga mkono taifa la Palestina katika vita visivyo na mlingano na utawala huo wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza.
29 Machi 2024
Ayatullah Khatami: Siku ya Quds itakuwa tofauti kabisa mwaka huu
Khatibu wa Swala ya Ijumaa iliyoswaliwa hapa Tehran hii leo ameashiria jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza na kusema kuwa, hadithi ya Siku ya Kimataifa ya Quds mwaka huu, itakuwa hadithi tofauti kabisa kutokana na hamasa na wingi wa watu watakaoshiriki matembezi ya siku hii.
29 Machi 2024
Wapalestina: Gati ya muda inayotaka kujenga Marekani Ghaza ni "Bandari ya Uvamizi"
Wapalestina wanaielezea gati ya muda inayojengwa na Marekani kwenye pwani ya mji wa Ghaza kuwa ni "bandari ya uvamizi na ukaliaji ardhi kwa mabavu".
29 Machi 2024
Wamorocco waungana na Wajordan kuzitaka serikali zao zivunje uhusiano na Israel
Maelfu ya watu wameandamana katika nchi za Jordan na Morocco kuonyesha mshikamano na Wapalestina ambao wamekuwa wakikabiliwa na vita vya kinyama vya mauaji ya kimbari vinavyoendeshwa na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa takriban miezi sita sasa, sambamba na kutoa wito kwa serikali zao wa kuvunja uhusiano na utawala huo ghasibu.