Main Title
27 Machi 2024
Kiongozi Muadhamu: Muqawama usio na kifani wa vikosi vya Muqawama na watu wa Ghaza umeutukuza Uislamu
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema, Muqawama usio na kifani wa vikosi vya Muqawama na watu wa Ghaza umeutukuza Uislamu.
27 Machi 2024
Safari ya pili ya Haniyeh mjini Tehran baada ya operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa
Ismail Haniyeh, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Hamas, aliwasili Jumanne ya jana mjini Tehran ikiwa ni safari yake ya pili baada ya operesheni ya Kimbunga cha Al Aqsa katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu na utawala ghasibu wa Israel.
27 Machi 2024
Haniya: Azimio la Baraza la Usalama linaonesha Israel imetengwa duniani
Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema utawala wa Kizayuni wa Israel umetengwa vibaya na dunia kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa; siku moja baada ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupasisha azimio la kutaka kusitishwa mara moja mapigano huko Gaza.
27 Machi 2024
Iran yazitaka IPU, NAM kufanya juhudi za kusitisha vita Gaza
Iran imetoa mwito kwa Jumuiya ya Kimataifa ya Mabunge (IPU) na Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Upande Wowote (NAM) kuchukua hatua za maana na za kivitendo kusitisha mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
27 Machi 2024
Kuendelea kushambuliwa na kuzingirwa hospitali za Gaza na utawala wa Kizayuni
Licha ya wasiwasi mkubwa na maonyo ya mara kwa mara ya viongozi wa nchi mbalimbali na taasisi za kimataifa, utawala wa Kizayuni bado unaendelea kushambulia na kuzizingira hospitali za Gaza.
27 Machi 2024
Israel yapuuza azimio la Baraza la Usalama, yadondosha mabomu Rafah
Jeshi katili la Israel limeendelea kuushambulia kwa mabomu mji wa Rafah wa kusini mwa Ukanda wa Gaza, licha ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupasisha azimio la kusimamisha vita huko Gaza baada ya miezi sita ya mashambulizi ya jeshi la utawala huo wa Kizayuni katika eneo hilo.
27 Machi 2024
Yemen yafanya mashambulizi 6 dhidi ya US, UK na Israel
Vikosi vya Jeshi la Yemen vimefanya mashambulizi sita dhidi ya meli za Marekani, Uingereza na utawala haramu wa Israel, ukiwa ni muendelezo wa operesheni za kuwaunga mkono wananchi madhulumu wa Palestina na kujibu uvamizi wa Washington na London dhidi ya Yemen.
27 Machi 2024
Mateka wa Kipalestina waongezeka pakubwa katika jela za utawala wa Kizayuni
Klabu ya Mateka wa Palestina imetangaza kuwa kuna ongezeko kubwa sana la mateka wa Kipalestina wanashikiliwa katika jela za utawala wa Kizayuni bila ya kuhukumiwa.
25 Machi 2024
'Siku ya Kimataifa ya Quds ni siku ya kutangaza mshikamano na Wapalestina'
Mwanaharakati mmoja na mtafiti wa Chuo Kikuu raia wa Nigeria amewataka wananchi wa nchi za Afrika wajitokeze kwa wingi kwenye maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Quds ambayo ni Ijumaa ya mwisho ya mwezi huu mtukufu wa Ramadhani akisisitiza kuwa hiyo ni siku ya kutangaza uungaji mkono kwa wananchi madhlumu wa Palestina wanaofanyiwa ukatili wa kutisha na Israel.
25 Machi 2024
Matteo Salvini: Macron mpiga ngoma ya vita ni "hatari" kwa Ulaya
Naibu Waziri Mkuu wa Italia, Matteo Salvini, amesema Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, ni "mchochezi wa vita" na ni "hatari" kwa Ulaya kwa kuendelea kushikamana na msimamo wake wa kutuma wanajeshi wa nchi kavu wa nchi za Magharibi huko Ukraine.
25 Machi 2024
Guterres akiri kashfa ya kimaadili ya utawala wa Kizayuni katika kuzuia misaada ya kibinadamu kuingia Gaza.
Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ametembelea kivuko cha Rafah (kati ya Ukanda wa Gaza na Misri), katika mwezi wa sita wa mauaji ya halaiki ya utawala wa Kizayuni huko Gaza, na kukitaja kitendo cha utawala huo wa Kizayuni cha kuzuia misaada ya kibinadamu kuingia Gaza kuwa ni "kashfa ya kimaadili".
25 Machi 2024
Mkutano wa Umoja wa Mabunge unaendelea Geneva kwa kuhudhuriwa na Iran
Mkutano wa Umoja wa Mabunge Duniani, kama chombo kikubwa zaidi cha utungaji sheria chenye nchi wanachama zaidi ya 180, ukiwemo ujumbe kutoka Iran unafanyika mjini Geneva Uswisi kwa kauli mbiu ya "Diplomasia ya Bunge, Ujenzi wa Daraja la Amani na Maelewano".
25 Machi 2024
Wairani waandamana kulaani jinai za Israel katika Ukanda wa Gaza
Wananchi wa Iran wamefanya maandamano makubwa katika sehemu mbalimbali za nchi ukiwemo mji mkuu Tehran, kutangaza mshikamano na wananchi madhulumu wa Palestina wanaoendelea kuuawa, sambamba na kulaani jinai za kutisha zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
25 Machi 2024
Iran na Oman zasisitizia udharura wa kukomeshwa mara moja jinai za Israel Ghaza
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Oman wamefanya mazungumzo ya simu na kutilia mkazo wajibu wa kuchukuliwa hatua za haraka na jamii ya kimataifa za kukomesha jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya wananchi madhlumu na wasio na ulinzi wa Palestina hasa wa Ukanda wa Ghaza.
25 Machi 2024
Shirikisho la Soka la Iran limekaribisha pendekezo la Wapalestina la kuwekewa vikwazo Shirikisho la soka la Israel
Mkuu wa Shirikisho la Soka la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemtumia barua k Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), akikaribisha mpango uliopendekezwa wa Shirikisho la Soka la Palestina kuhusu kuwekewa vikwazo Shirikisho la Soka la utawala wa Kizayuni.
25 Machi 2024
Kufeli propaganda dhidi ya Hamas na kuongezeka umaarufu wa harakati hiyo huko Gaza
Licha ya kuenea propaganda sumu za vyombo vya habari vya Magharibi na baadhi ya nchi za Kiarabu, lakini kura za uchunguzi wa maoni zinaonyesha kuwa wakazi wengi wa Ukanda wa Gaza wanaridhishwa na utendaji wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu wa Palestina (Hamas).
25 Machi 2024
Shahidi: Wanajeshi wa Israel wamewabaka wanawake wa Kipalestina kabla ya kuwaua katika Hospitali ya al-Shifa
Mwanamke wa Kipalestina amesimulia matukio ya kutisha baada ya wanajeshi wa Israel kuvamia Hospitali ya al-Shifa katika mji wa Gaza wiki iliyopita, na kusema kuwa wanajeshi wa utawala huo ghasibu wanawabaka wanawake wa Kipalestina kabla ya kuwaua.
25 Machi 2024
Saraya Al-Quds yaangamiza Afisa mmoja na wanajeshi 3 wa Israel katika shambulizi la kuvizia huko Tulkarm
Brigedi za al Quds (Saraya al Quds) Batalioni ya Tulkarm imetangaza kuwa wanachama wake wamevamia gari lililokuwa na afisa mmoja na wanajeshi watatu wa Israel kaskazini mwa Tulkarm katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kuwaangamiza wote.
25 Machi 2024
Al-Azhar: Hatua za kimataifa mkabala wa jinai za Israel Ukanda wa Gaza zinakatisha tamaa
Imamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Al Azhar cha Misri amesema kuwa radiamali za jamii ya kimataifa mkabala wa vita vya Israel dhidi ya Gaza zinakatisha tamaa.
24 Machi 2024
Wasiwasi wa Marekani kuhusu muungano wa Iran, Russia na China
Kamanda wa Kamandi Kuu ya Jeshi la Marekani (CENTCOM) Jenerali Michael E. Kurilla amebainisha wasiwasi wake kuhusu kuongezeka kwa ushirikiano kati ya Iran, China na Russia na kudai kuwa ushirikiano wa nchi hizo utakuwa na"matokeo mabaya ya kimataifa".