Main Title
2 Aprili 2024
Askari wa Israel wakiri, wengi waliowaua Ghaza kama 'magaidi' ni raia wa kawaida
Maafisa na askari wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel wamekiri kuwa akthari ya vifo vilivyoelezewa na jeshi hilo kuwa ni vya kuua "magaidi" wakati wa vita vyake dhidi ya Ukanda wa Ghaza, kiukweli hasa ni vya mauaji ya raia wa kawaida.
2 Aprili 2024
Baada ya kufanya unyama mkubwa kwa majuma 2, jeshi la Israel laondoka Hospitali ya Al-Shifa
Jeshi la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel limeondoka ndani ya Hospitali ya Al-Shifa na maeneo ya jirani magharibi mwa Mji wa Ghaza mapema jana Jumatatu na kuacha majeruhi wengi na uharibifu mkubwa katika hospitali hiyo na viunga vyake.
2 Aprili 2024
Jeshi la Kizayuni laendeleza mashambulizi ya kinyama katika makazi ya raia Ghaza
Sambamba na kukaribia mwezi wa sita wa mashambulizi ya kikatili na kinyama ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Ghaza, hujuma za mashambulio ya mabomu na makombora ya jeshi la utawala huo katika maeneo ya makazi ya watu yangali yanaendelea.
2 Aprili 2024
Kwa mara nyingine, Oman yalaani shambulio la Israel kwenye ubalozi wa Iran
Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman amelaani shambulio la kigaidi lililofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjiini Damascus Syria. Kabla ya hapo Wizara ya Mambo ya Nje ya Oman iliikuwa imetoa taarifa rasmi ya kulaani shambuliizi hilo la kigaidi.
1 Aprili 2024
Ufaransa, Misri na Jordan zapinga shambulio la Rafah na kuunga mkono usitishaji vita Gaza
Mkutano wa pande tatu wa mawaziri wa mambo ya nje wa Misri, Jordan na Ufaransa ulifanyika Jumamosi Cairo, mji mkuu wa Misri, kuhusiana na matukio ya hivi karibuni katika vita vya Gaza na mashauriano ya kusitisha mapigano hayo.
1 Aprili 2024
Wataalamu na wanasiasa: Israel haidhibitiki, asiyeiadhibu ni mshirika katika uhalifu
Wataalamu na wanasiasa wanasema Israel imefikia hatua ya unazi ambayo haiwezi kuvumiliwa na kwamba Marekani, nchi za Magharibi na Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ni washirika katika jinai zinazofanywa na utawala huo zikiwemo nchi za Kiarabu ambazo hazikuchukua hatua yoyote kuiadhibu Israel baada ya uamuzi wa hivi karibuni wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wa ulazima wa kusitisha mapigano mara moja huko Gaza.
1 Aprili 2024
UNICEF yaonya kuhusu hali ya kutisha ya vita kwa watoto wa Ghaza
Msemaji wa Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuhudumia Watoto ameonya kuhusu hali mbaya na ya kutisha waliyo nayo watoto wa ukanda wa Ghaza ambao wanateseka kwa mambo mengi ikiwemo njaa na mashambulizi ya mfululizo ya wanajeshi katili wa utawala wa Kizayuni.
1 Aprili 2024
Shambulizi la Moscow... Russia yaitaka Kiev kumkabidhi mkuu wa usalama
Russia imeitaka Ukraine kuwakabidhi raia wake kadhaa, akiwemo Mkuu wa Idara ya Usalama ya nchi hiyo, kwa madai kwamba walihusika na vitendo vya "kigaidi" katika ardhi ya Russia, suala ambalo Kiev imelitaja kuwa takwa"lisilo na thamani".
1 Aprili 2024
Corbyn: Kuendelea Uingereza kuipa Israel silaha kunaifanya mshirika katika mauaji ya kimbari Gaza
Kiongozi wa zamani wa chama cha Labour nchini Uingereza amezikosoa nchi za Magharibi - hasa Marekani na Uingereza - zinazoendelea kuipatia Israel silaha za kuwaua Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, na kusema kuwa nchi hizo zinakiuka sheria za kimataifa.
1 Aprili 2024
Msaada mpya wa silaha wa Marekani kwa Israel wa kufanyia mauaji makubwa zaidi ya kimbari ya Wapalestina
Sambamba na juhudi zinazofanywa kimataifa kwa lengo la kusimamisha mauaji ya kimbari ya Wapalestina yanayofanywa na utawala wa Kizayuni; na mashinikizo yanayotolewa kwa utawala huo uhakikishe unaruhusu kuingizwa misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Ghaza, duru za habari za Marekani zimeripoti kuwa serikali ya Washington imeidhinisha kupatiwa Israel shehena mpya ya silaha za kisasa ili kuweza kuua idadi kubwa zaidi ya Wapalestina.
1 Aprili 2024
Kan'ani: Wazayuni wanafanya jinai Gaza mbele ya macho ya walimwengu
Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema jinai za kutisha za kivita zinazofanywa na Wazayuni eneo la Ukanda wa Gaza huko Palestina zinaendelea mbele ya macho ya walimwengu.
1 Aprili 2024
Rais Raisi ahimiza kutekelezwa kivitendo mafundisho ya Qur'ani Tukufu
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kuzingatia mafundisho wa Qur'ani Tukufu katika nyuga zote ni jambo la dharura kwa ajili ya mafanikio ya wanadamu ya duniani na Akhera.
1 Aprili 2024
Iran na Misri zataka kufanyike juhudi madhubuti za kuizuia Israel isiuvamie mji wa Rafah
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Misri wametoa mwito wa kuchukuliwa hatua za maana kimataifa ili kuzuia mashambulizi ya kivamizi ya utawala wa Kizayuni katika mji wa Rafah wa kusini mwa Ukanda wa Ghaza.
1 Aprili 2024
Raisi: Leo hii utawala wa Kizayuni unatumia vibaya mizozo baina ya Waislamu
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, lau kama nchi za Waislamu zingeacha kuitegemea Marekani na madola ya kibeberu na badala yake kuishi kwa mujibu wa mafundisho ya Qur'ani Tukufu, basi leo hii wananchi wa Ghaza na Wapaletina wasingtelikuwa wananyanyaswa na utawala wa Kizayuni wa Israel.
1 Aprili 2024
Makundi ya ukombozi ya Palestina: Hatutaruhusu jeshi lolote la kimataifa au la Kiarabu kuingia Gaza
Makundi ya ukombozi ya Wapalestina yametangaza kuwa jeshi lolote la kimataifa au la Kiarabu litakaloingia katika Ukanda wa Gaza halikubaliki na litatambuliwa kuwa ni jeshi vamizi.
1 Aprili 2024
Kwa mara nyingine, Hizbullah yazitwanga kwa mizinga kambi za kijeshi za Israel
Wanamapambano wa Kiislamu wa nchini Lebanon kwa mara nyingine wamezitwanga kwa mizinga kambi za kijeshi za utawala wa Kizayuni wa Israel kujibu jinai na mauaji ya umati yanayofanywa na Wazayuni huko Ghaza, Palestina.
1 Aprili 2024
Hamas: Kuanzisha maeneo ya kunyonga watu huko Gaza ni uhalifu wa kikatili wa kivita
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema kwamba, kilichofichuliwa na vyombo vya habari vya Israel kuhusu hatua ya jeshi la utawala huo ya kuanzishwa "maeneo ya kunyonga watu" katika Ukanda wa Gaza, ambapo mtu yeyote anayetembea katika maeneo hayo anauawa, ni jinai ya kikatili ya kivita.
31 Machi 2024
Zelensky aonya: Bila msaada wa kijeshi wa Marekani, Ukraine italazimika kurudi nyuma
Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine amesema iwapo nchi yake haitopatiwa msaada wa kijeshi ulioahidiwa na Marekani ambao kwa sasa umezuiwa kutokana na mizozo iliyomo ndani ya Kongresi ya nchi hiyo italazimika kurudi nyuma katika vita na Russia hatua kwa hatua.
31 Machi 2024
Watu masikini na wakimbizi wafukuzwa Paris kabla ya Olimpiki
Takriban wakimbizi 500 na watu masikini wasio na makazi wamehamishwa kwa nguvu kutoka mji mkuu wa Ufaransa na kupelekwa maaeneo ya vijijini na miji midogo nchini humo huku Paris ikijiitayarisha kuandaa Olimpiki ya Majira ya joto ya 2024 mnamo Julai na Agosti.
31 Machi 2024
Wananchi wa Uturuki washiriki katika uchaguzi muhimu wa serikali za mitaa
Vituo vya kupigia kura nchini Uturuki vilifunguliwa mapema leo asubuhi kuruhusu wananchi kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotajwa kuwa ni mtihani muhimu kwa Rais Recep Tayyip Erdogan wa nchi hiyo. Weledi wa mambo wanasema kuwa Rais wa Uturuki anakabiliwa na kibarua kigumu ili kuyarejesha maeneo muhimu ya mijini aliyoshindwa na upinzani miaka mitano iliyopita.