Main Title

source :
Jumanne

2 Aprili 2024

14:41:18
1448529

Naibu Katibu Mkuu wa UN: Jaribio la kuitenga UNRWA lazima likome

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na uratibu wa misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura Martin Griffiths amesema shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA ni uti wa mgongo wa operesheni za kibinadamu Ghaza, hivyo jaribio la kulitenga shirika hilo lazima likome.

source :
Jumanne

2 Aprili 2024

14:40:49
1448528

Iran: Uchunguzi wa kimataifa ufanyike kuhusu jinai ilizofanya Israel katika Hospitali ya Al-Shifa

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesisitizia ulazima wa kufanyika uchunguzi wa kimataifa kuhusiana na uharibifu, utesaji na mauaji yaliyofanywa na jeshi la Kizayuni katika Hospitali ya Al-Shifa huko Ukanda wa Ghaza.

source :
Jumanne

2 Aprili 2024

14:40:20
1448527

Shambulio la kigaidi la Israel katika ubalozi mdogo wa Iran Damascus lalaaniwa kimataifa

Russia, Pakistan, Oman, Imarati na Qatar zimeungana na mataifa mengine kuulaani utawala haramu wa Kizayuni wa Israel kufuatia shambulio la kigaidi ulilofanya utawala huo katika ubalozi mdogo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Damascus, Syria.

source :
Jumanne

2 Aprili 2024

14:39:53
1448526

Balozi wa Iran Syria: Tutajibu mapigo kwa Israel sawa na ilivyoshambulia ubalozi wetu mdogo

Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Syria amesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu itajibu mapigo sawa na utawala wa Kizayuni wa Israel ulivyoshambulia ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Syria.

source :
Jumanne

2 Aprili 2024

14:39:25
1448525

Iran: Utawala wa Kizayuni ni tishio kwa usalama na amani ya dunia nzima

Mwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa na taasisi nyinginezo za kimataifa huko Geneva Uswisi amelaani vikali jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel katika ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus Syria na kusema kuwa Israel ni utawala unaohatarisha usalama wa dunia nzima na unapuuza kikamilifu hati ya Umoja wa Mataifa.

source :
Jumanne

2 Aprili 2024

14:39:03
1448524

Rais Raisi: Wazayuni kamwe hawatofikia malengo yao haramu

Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amezungumzia jinai na ugaidi uliofanywa jana Jumatatu na utawala wa Kizayuni wa kushambulia ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus Syria na kusema kuwa, Wazayuni wanapaswa kutambua kwamba ugaidi wao wa kinyama kama huo hauwezi kuwafanikishia malengo yao maovu.

source :
Jumanne

2 Aprili 2024

14:38:42
1448523

Kiongozi Muadhamu: Iran itaufanya utawala wa Israel ujutie uhalifu nchini Syria

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametuma salamu za rambirambi kufuatia kuuawa shahidi Majenerali walioongoka wa Kiislamu katika shambulio la utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran nchini Syria na kusisitiza kwamba: "Taifa la Iran litawafanya Wazayuni wajutie jinai hiyo na jinai zingine kama hiyo."

source :
Jumanne

2 Aprili 2024

14:38:19
1448522

Sababu za utawala wa Kizayuni kulazimisha vita katika upande wa kaskazini

Yoav Gallant, Waziri wa Vita wa utawala wa Kizayuni, amesema kwamba utawala huo haramu utapanua operesheni zake za kijeshi katika eneo la kaskazini la ardhi zinazokaliwa kwa mabvu na kushambulia kila sehemu ya Beirut na Damascus ambapo Hizbullah ya Lebanon inaendeshea shughuli zake.

source :
Jumanne

2 Aprili 2024

14:37:45
1448521

Askari wa Israel wakiri, wengi waliowaua Ghaza kama 'magaidi' ni raia wa kawaida

Maafisa na askari wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel wamekiri kuwa akthari ya vifo vilivyoelezewa na jeshi hilo kuwa ni vya kuua "magaidi" wakati wa vita vyake dhidi ya Ukanda wa Ghaza, kiukweli hasa ni vya mauaji ya raia wa kawaida.

source :
Jumanne

2 Aprili 2024

14:37:11
1448519

Baada ya kufanya unyama mkubwa kwa majuma 2, jeshi la Israel laondoka Hospitali ya Al-Shifa

Jeshi la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel limeondoka ndani ya Hospitali ya Al-Shifa na maeneo ya jirani magharibi mwa Mji wa Ghaza mapema jana Jumatatu na kuacha majeruhi wengi na uharibifu mkubwa katika hospitali hiyo na viunga vyake.

source :
Jumanne

2 Aprili 2024

14:36:41
1448518

Jeshi la Kizayuni laendeleza mashambulizi ya kinyama katika makazi ya raia Ghaza

Sambamba na kukaribia mwezi wa sita wa mashambulizi ya kikatili na kinyama ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Ghaza, hujuma za mashambulio ya mabomu na makombora ya jeshi la utawala huo katika maeneo ya makazi ya watu yangali yanaendelea.

source :
Jumanne

2 Aprili 2024

14:36:02
1448517

Kwa mara nyingine, Oman yalaani shambulio la Israel kwenye ubalozi wa Iran

Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman amelaani shambulio la kigaidi lililofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjiini Damascus Syria. Kabla ya hapo Wizara ya Mambo ya Nje ya Oman iliikuwa imetoa taarifa rasmi ya kulaani shambuliizi hilo la kigaidi.

source :
Jumatatu

1 Aprili 2024

14:22:58
1448218

Ufaransa, Misri na Jordan zapinga shambulio la Rafah na kuunga mkono usitishaji vita Gaza

Mkutano wa pande tatu wa mawaziri wa mambo ya nje wa Misri, Jordan na Ufaransa ulifanyika Jumamosi Cairo, mji mkuu wa Misri, kuhusiana na matukio ya hivi karibuni katika vita vya Gaza na mashauriano ya kusitisha mapigano hayo.

source :
Jumatatu

1 Aprili 2024

14:22:16
1448217

Wataalamu na wanasiasa: Israel haidhibitiki, asiyeiadhibu ni mshirika katika uhalifu

Wataalamu na wanasiasa wanasema Israel imefikia hatua ya unazi ambayo haiwezi kuvumiliwa na kwamba Marekani, nchi za Magharibi na Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ni washirika katika jinai zinazofanywa na utawala huo zikiwemo nchi za Kiarabu ambazo hazikuchukua hatua yoyote kuiadhibu Israel baada ya uamuzi wa hivi karibuni wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wa ulazima wa kusitisha mapigano mara moja huko Gaza.

source :
Jumatatu

1 Aprili 2024

14:21:40
1448216

UNICEF yaonya kuhusu hali ya kutisha ya vita kwa watoto wa Ghaza

Msemaji wa Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuhudumia Watoto ameonya kuhusu hali mbaya na ya kutisha waliyo nayo watoto wa ukanda wa Ghaza ambao wanateseka kwa mambo mengi ikiwemo njaa na mashambulizi ya mfululizo ya wanajeshi katili wa utawala wa Kizayuni.

source :
Jumatatu

1 Aprili 2024

14:21:19
1448215

Shambulizi la Moscow... Russia yaitaka Kiev kumkabidhi mkuu wa usalama

Russia imeitaka Ukraine kuwakabidhi raia wake kadhaa, akiwemo Mkuu wa Idara ya Usalama ya nchi hiyo, kwa madai kwamba walihusika na vitendo vya "kigaidi" katika ardhi ya Russia, suala ambalo Kiev imelitaja kuwa takwa"lisilo na thamani".

source :
Jumatatu

1 Aprili 2024

14:20:15
1448214

Corbyn: Kuendelea Uingereza kuipa Israel silaha kunaifanya mshirika katika mauaji ya kimbari Gaza

Kiongozi wa zamani wa chama cha Labour nchini Uingereza amezikosoa nchi za Magharibi - hasa Marekani na Uingereza - zinazoendelea kuipatia Israel silaha za kuwaua Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, na kusema kuwa nchi hizo zinakiuka sheria za kimataifa.

source :
Jumatatu

1 Aprili 2024

14:19:39
1448213

Msaada mpya wa silaha wa Marekani kwa Israel wa kufanyia mauaji makubwa zaidi ya kimbari ya Wapalestina

Sambamba na juhudi zinazofanywa kimataifa kwa lengo la kusimamisha mauaji ya kimbari ya Wapalestina yanayofanywa na utawala wa Kizayuni; na mashinikizo yanayotolewa kwa utawala huo uhakikishe unaruhusu kuingizwa misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Ghaza, duru za habari za Marekani zimeripoti kuwa serikali ya Washington imeidhinisha kupatiwa Israel shehena mpya ya silaha za kisasa ili kuweza kuua idadi kubwa zaidi ya Wapalestina.

source :
Jumatatu

1 Aprili 2024

14:18:59
1448212

Kan'ani: Wazayuni wanafanya jinai Gaza mbele ya macho ya walimwengu

Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema jinai za kutisha za kivita zinazofanywa na Wazayuni eneo la Ukanda wa Gaza huko Palestina zinaendelea mbele ya macho ya walimwengu.

source :
Jumatatu

1 Aprili 2024

14:18:30
1448211

Rais Raisi ahimiza kutekelezwa kivitendo mafundisho ya Qur'ani Tukufu

Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kuzingatia mafundisho wa Qur'ani Tukufu katika nyuga zote ni jambo la dharura kwa ajili ya mafanikio ya wanadamu ya duniani na Akhera.