Polisi nchini Burundi wamefyatua risasi kwa waandamanaji leo wakati rais Pierre Nkurunziza akikaidi mbinyo wa kimataifa kuacha juhudi zake za kuwania urais kwa kipindi cha tatu, kabla ya mkutano wa kikanda kuzungumzia mzozo huo.
Mtu mmoja ameuwawa katika ghasia hizo mpya na polisi katika mitaa ya mji mkuu wa Burundi, Bujumbura , wakati watu wengine wawili wameripotiwa kuuwawa usiku katika mripuko wa guruneti.
Idadi ya vifo sasa imefikia watu 20 waliouwawa katika wiki zaidi ya mbili za maandamano dhidi ya serikali na yanakuja wakati viongozi wa mataifa ya Afrika mashariki wanajitayarisha kwa mkutano wa dharura nchini tanzania kesho.
Zaidi wa Waburundi 50,000 wameikimbia nchi hiyo wakikimbialia katika nchi jirani tangu ghasia hizo kuanza.
Rais Joseph Kabila wa jamhuri ya kidemokrasi ya Congo, makamu wa rais wa Afrika kusini Cyril Ramaphosa na mwanadiplomasia wa ngazi ya juu wa Marekani kwa ajili ya Afrika Linda Thomas-Greenfield pia wanatarajiwa kuhudhuria mkutano huo.